RUVU SHOOTING YAMNASA MOMBEKI
Klabu ya Ruvu Shooting
ya Pwani, imeamua kumwaga nyota watano kwa mpigo katika harakati za kutafuta
mastraika, safu ambayo imewasumbua kwa muda mrefu tangu kuondoka kwa Elias
Maguli aliyetimkia Simba.
Ofisa Habari wa Ruvu,
Masau Bwire, alisema nyota hao tayari wameanza majaribio tangu juzi Jumatatu
ambapo wataangalia wenye uwezo zaidi kabla ya kuwapa saini.
Bwire amesema kuwa
wameamua kuvalia njuga safu hiyo kwani ndiyo iliyoonyesha matatizo zaidi katika
mechi saba za mzunguko wa kwanza.
Imeelezwa
kuwa mshambuliaji wa zamani wa Simba,
Betram Mwombeki amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Ruvu Shooting.
Mwombeki
ambaye aliachwa na Simba na baadaye kwenda Oman kufanya majaribio ambako
imeelezwa hakufuzu, amesaini kuichezea Ruvu Shooting leo.
Maana
yake, mshambuliaji huyo ataanza kuonekana kwenye mechi za Ligi Kuu Bara
zitakazoanza tena Desemba 26, mwaka huu.
THE EXPRESS YA UGANDA KUZIPIMA SIMBA, YANGA KABLA YA MTANI JEMBE
TIMU ya soka ya The Express
ya Uganda inatarajia kuwasili nchini kesho kwa ajili ya kucheza mechi ya
kirafiki ya kimataifa na timu za Simba na Yanga.

Amesema ni fursa nzuri kwa
makocha wa pande zote mbili kuangalia upungufu kwenye vikosi vyao kabla ya
mechi yao ya Desemba 13.Wakuganda amesema ameshafanya mazungumzo na pande zote
mbili za uongozi wa Simba na Yanga na wote wamekubali kucheza mechi hiyo ya
kirafiki ya kimataifa.
Kipindi hiki cha usajili wa
dirisha dogo Simba ilikuwa ikifanya mazungumzo na mchezaji Dan Ssemkuruma
ambaye anatarajiwa kuwasili nchini leo kwa ajili ya kumalizana na klabu hiyo
kutoka mitaa ya Msimbazi.Kwa wachezaji wa ndani Simba inaonyatia kwa sasa ni
Nurdin Choma wa Prisons ya Mbeya anayecheza nafasi ya beki wa kati na beki wa
kulia Salum Kimenya wa Prisons pia. Simba pia inataka kuwabomoa Mbeya City kwa
kumsajili kiungo mshambuliaji Deus Kaseke.
Endapo Simba itamalizana na
wachezaji hao, Ijumaa wanaweza kuonekana uwanjani. Yanga itatumia nafasi hiyo
kumtambulisha kiungo wao mpya Mbrazil Emerson De Oliveira Neves Roque.
AZAM FC SASA KUSAJILI
MUIVORY COAST MWINGINE
KLABU ya
Azam FC imeonekana kunogewa na wachezaji wa Ivory Coast na sasa ina mpango wa
kumsajili Sanaly Bamba kuongeza nguvu kwenye kikosi hicho chenye makazi yake
Chamanzi.
Tayari
Azam ina wachezaji watatu wa Ivory Coast ambao ni Pascal Wawa aliyekuwa
akikipiga El Mereikh ya Jamhuri ya Sudan, Kipre Tchetche na Kipre Bolou.
Mchezaji huyo tayari yupo nchini kwa takriban wiki mbili akifanya mazoezi.
Alitokea Nigeria alipokuwa akicheza soka.
Meneja wa
Azam FC Jemedari Said alisema Bamba atasajiliwa iwapo Kocha Mkuu wa klabu hiyo
Joseph Omong na msaidizi wake George Nsimbe ‘Best’ watakubali kiwango chake.
Alisema
Nsimbe ndio kwanza ameanza kazi tangu juzi hivyo anahitaji kumwona mchezaji
huyo kisha kuungana na Omong katika maamuzi ya pamoja.
Wakati
Nsimbe anatua nchini hivi karibuni alisema Uganda kuna wachezaji wengi wazuri
wenye vipaji hivyo atatumia nafasi yake kuwasajili kwenye timu hiyo iweze
kufanya vizuri.
Klabu
hiyo ya Azam FC ilionesha nia ya kumsajili mshambuliaji wa Mali Mohamed Traore
aliyekuwa akikipiga katika klabu ya El Mereikh lakini mpaka sasa haijawa wazi
kama watamsajili ama la.
Azam
inasajili kujiimarisha kutetea taji lake la Ligi Kuu, haina mwenendo mbaya
kwenye ligi kwani inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 13 sawa na Yanga
iliyo nafasi ya pili. Kinara wa ligi hiyo ni Mtibwa Sugar ikikaa kileleni kwa
pointi 15.
No comments:
Post a Comment