HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 15 December 2014

WAZIRI GHASIA ATOA UFAFANUZI KUHUSU DOSARI ZILIZOJITOKEZA KWENYE UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA NA VITONGOJI.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi)  Hawa Gasia

SERIKALI  nchini imekili Uchaguzi uliomalizika jana  wa Serikali za Mitaa ulikuwa na Dosari katika baadhi ya Maeneo mbalimbali nchini na kusema itawachukulia Hatua kali za Watendaji Halmashauri Mbalimbali waliopelekea kuwepo na Dosari hizo.
Pia Licha ya kuwa na Dosari lakini Badao Serikali imesema uchaguzi huo umefanikiwa kwa asilimia 98,Tofautisha na Miaka mingine.

Hayo  yemesemwa leo Jijini Dar Es Salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi)  Hawa Gasia wakati wa Mkutano na Waandishi ili kuzungumzia uchaguzi huo wa Serikali za Mitaa ambapo pamoja na Mambo Mengine Waziri Gasia alikili kuwepo na Dosari kwenye Vituo mbalimbali vya kupiga kura  katika baadhi ya Kata,Vijiji,Mtaa au Vitongoji 

Waziri Gasia alizitaja Dosari hizo ambazo  ni kukosekana na Ujio wa Vifaa vya Kupigia Kura,Kasoro za karatasi za kupigia kura,wapiga kura majina yao kutokuwepo katika vituo pamoja na kuwepo na udangachifu kutoka kwa wapiga kura.

Vilevele Waziri Gasia alisema Halmashauri na Maeneo yenye Kasoro ambayo hayakufanya Uchaguzi,yatarudia uchaguzi huo ndani ya Siku (7) kama kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa zinavyoelekeza.
Aidha,Waziri Gasia aliitaja Mikoa ambayo Dosari zilijitokeza na kupelekea kuhailishwa kwa  uchaguzi huo katika baadhi ya Kata, vitongoji na Vijiji ni,  Kilimanjaro , Manyara,Morogoro,Shinyanga,Simiyu,Kigoma,Mwanza,Tabora,Tanga,Mara,Rukwa,Dar Es Salaam,pmoja na Mkoa wa Pwani.

Waziri Gasia aliongeza kuwa kwa ujumla Halmashauri ambazo hazinadosari ni 145 kati 162 zilizofanya uchaguzi ambapo Halmashauri tatu kati ya hizo hazikufanya Uchaguzi kabisa kutokana na kucheleweshwa kwa Vifaa.
Hatahivyo Waziri Gasia aliziagiza Halmashauri hizo uchaguzi kufanya haraka ndani ya siku 7 na vilevile Wizara hiyo ya TAMISEMI itawachukuli hatua kali za watendaji waliopelekea Dosari hizo.

 “Tumeitaka Mikoa Iwasilishe Taarifa rasmi na  kamiilifu kuhusu Kilichojitokeza katika Halmashauri hizo na Wizara itachambua taarifa hizo ili kubaini wote waliosababisha kasoro wachukuliwe hatua stahiki ikiwemo kusimamisha kazi,kukatwa mishahara,pamoja na kufukuzwa kazi”alisema Waziri Gasia.
Waziri Gasia aliongeza kuwa licha ya uchaguzi wa mwaka huu wa Serikali za Mitaa kuwepo na Changamoto mbalimbali lakini serikali imefanikiwa uchaguzi huu kwa asilimia 98 tofautisha na miaka mingine.

No comments:

Post a Comment