HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 15 December 2014

"bofya hapa" KUPATA TAARIFA ZA MWISHO ZA USAJILI WA DIRISHA DOGO Tz BARA 2014/15



MWADUI FC YA JULIO YAKAMILISHA USAJILI, YAMTWAA BEKI WA SIMBA





Mwadui FC imeendelea kujiimarisha ambapo jana kabla dirisha la usajili halijafungwa imefanya usajili wa kushangaza.Mwadui inayoshiriki daraja la kwanza, imefanikiwa kumsajili kiungo wa Coastal Union, Razak Khalfan.

Katika hatua nyingine  Mwadui FC imewatema wachezaji wawili wakongwe Salum Sued Kusi na Victor Costa.Kusi aliwahi kung'ara na Yanga pamoja na Mtibwa Sugar kama ilivyo kwa Costa aliyewahi kufanya vizuri na Mtibwa kabla ya kung'ara zaidi na Simba.

 
Imeripotiwa kuwa Mwadui FC pia imemnsa kiungo mwenye kasi Uhuru Selemani.Kocha Mkuu wa Mwadui FC, Jamhuri Kiwhelo 'Julio' amethibitisha kumtwaa Uhuru.

Klabu hiyo pia imefanikiwa kumnasa beki Joram Mgeveke wa Simba.
Beki huyo anayekipiga katika kikosi cha Taifa Stars amejiunga na Mwadui FC jana kwa mkopo.Mwadui pia imemasajili Mohammed Mkweche.

EXCLUSIVE:...SIMBA YAFUNGA MKATABA NA BEKI KESSY WA MTIBWA SUGAR

Simba imefunga usajili rasmi kwa kumsajili beki wa kulia, Ramadhani Kessy kutoka Mtibwa Sugar.Kessy amejiunga na Simba jana baada ya kusaini mkataba wa kuichezea Simba kwa miezi 18.Kessy amesaini mkataba huo mbele ya Meneja wake, Athumani Tippo pamoja na Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu'.

Tetesi zaidi zinasema kuwa Simba imemsajili beki huyo kwa thamani ya shilingi milioni 30.

EXCLUSIVE; TAMBWE RASMI ASAINI YANGA.

Hayawi Hayawi, Hatimaye mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita, Amissi Tambwe amesaini Yanga.Tambwe amejiunga na Yanga jana ikiwa ni dakika chache baada ya Simba kumtema.

Mbele ya Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Yanga, Francis Kifukwe, Tambwe ameanguka kuitumikia Yanga kwa mwaka mmoja.

No comments:

Post a Comment