HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 15 December 2014

MAMIA YA WACONGOMANI WAPOTEZA MAISHA ZIWA TANGANYIKA




Miili ya watu wapatao 129 imepatikana kutoka Ziwa Tanganyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, baada ya feri kupinduka na kuzama mapema Ijumaa.

Waziri wa Uchukuzi nchini humo Laurent Sumba Kahozi amesema msako unaendelea kuwatafuta watu waliopotea katika ajali hiyo.
Wafanyakazi wa uokoaji waliwapata abiria wakielea katika maji Jumapili, wakiwa katika mapipa ya petroli na vifaa vingine.
Maboti katika eneo hilo mara nyingi hujazaa abiria na mizigo kupita kiasi na ajali kutokea ni jambo la kawaida

Habari zinasema ajali kama hiyo ni za kawaida katika eneo hilo kutokana na boti kujaa abiria na mzigo kupita kiasi.
Maboya ya kujiokoa mara nyingi hayamo katika maboti hayo na watu wengi hawawezi kuogelea.
  
Maafisa katika jimbo la Katanga wamesema upepo mkali na kujaza abiria na mizigo kupita kiasi kumesababisha boti MV Mutambala, kupinduka.

Wanawake na watoto ni miongoni mwa watu waliokumbwa na ajali hiyo ambayo ilitokea mapema Ijumaa asubuhi.
Taarifa za awali zilisema watu 26 wamekufa katika ajali hiyo.
Idadi ya watu walionusurika imetajwa kuwa watu 232, wengi wakiwa ni wanaume, amesema waziri wa uchukuzi katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment