HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 15 December 2014

COASTAL UNION KUJIPIMA NA MWADUI JUMATANO.





MABINGWA wa soka Tanzania Bara mwaka 1988 Coastal Union “Wagosi wa Kaya”inatarajia kucheza mechi ya kirafiki na timu ya Mwadui ya Shinyanga ikiwa ni sehemu ya maandalizi kwa timu zote kujiandaa na michuano wanayokabiliana nayo.

Mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa Jumatano ya wiki hii kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani lengo likiwa ni kukipa makali kikosi cha Coastal Union kujiwida na mechi yao ya Ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Tanzania Prison itakayochezwa kwenye uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.

Akizungumza leo,Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar Assenga amesema kuwa mechi hiyo ni miongoni mwa michezo mbalimbali ya kirafiki wanayocheza ili kuweza kukiimarisha kikosi hicho ambacho msimu huu kimepania kufanya makubwa kwenye michuano ya Ligi kuu soka Tanzania.

Assenga amesema kuwa timu ya Mwadau ya Shinyanga inatazamiwa kuwasili mkoani hapa Jumanne wiki hii tayari kwa ajili ya mchezo huo ambao unatazamiwa kuwa na upinzani mkali.

Hata hiyo aliwataka wadau wa soka mkoani hapa kujitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo huo ikiwemo kuangalia wachezaji ambao wamesajiliwa msimu huu kwa ajili ya michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara.

Hata hivyo alisema kuwa baada ya kumalizika mechi hiyo wataangalia
uwezekano wa kucheza mechi nyengine ya kirafiki kabla ya kutua jijini
Mbeya ambapo watakwenda kucheza mechi yao ya Ligi kuu.

No comments:

Post a Comment