WAZAZI na walezi nchini wametakiwa
kushirikiana na walimu wa shule za awali
ili kuibua, na kuendeleza na vipaji na vipawa vya watoto wao.
Rai
hiyo imetolewa na katibu mkuu wa chama cha wanajombe waishio Jijini Tanga
(uwanjota) bwana Bernard Goliama kwenye sherehe za kuwaaga watoto wa shule
awali ya Front Runner Day Care Centre iliyofanyika hivi karibuni kwenye hoteli ya Nyinda iliyopo eneo la Bombo
jijini Tanga.
Amesema
kila mzazi na mlenzi nchini awajibike kuendeleza watoto kwa ngazi ya elimu ya
awali ili Tanzania iwe na wataalam wengi waliyo na misingi imara ya masomo yenye faida kwa manufaa ya sasa na baadaye.
Hata
hivyo Goliama hakusita kuwapongeza na kudhamini walimu na uongozi wa shule ya
Front Runner Day Care Centre kwa jitihada ya kutoa elimu ya watoto hao ambao ni zaidi ya watoto
25 wamemaliza elimu hiyo ya awali kwa huu 2014.
Sambamba
na hayo watoto wa shule hiyo kwa kupitia risala waliyosoma wamewaomba wadau wa elimu kusaidiana na uongozi wa shule
kuwajengea uzio wa shule hiyo ili waweze kusoma na kucheza kwa utulivu , furaha
na amani.
No comments:
Post a Comment