HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 20 December 2014

KUTOKA TANGA: WATANZANIA WAOMBWA KUVISAIDIA VITUO VYA KULELEA WATOTO WENYE ULEMAVU.



WATANZANIA wameombwa kuvisaidia vituo vya kulelea watoto na vijana wenye ulemavu katika jamii ili kuzitatua changamoto mbalimbali zinazowakabili hususan umaskini uliokithiri kwa wazazi ambao ni wanawake waliotelekezwa na waume zao.

Hayo ameyasema mratibu wa kituo cha kuwalelea watoto na vijana wenye ulemavu katika jamii (Y D C P) kilichopo jijini TANGA William Henry wakati akitoa ufafanuzi wa changamoto inayowakabili kituoni hapo kwa wadau wakiwemo viongozi wa serikali na sekta mbalimbali katika semina ya siku mbili iliyofanyika kwa lengo la kuwapa viongozi hao uelewa juu ya changamoto inayowakabili.

Aidha amesema kutokana changamoto nyingi zinazowakabili ni vyema jamii ya watanzani iwaunge mkono ili kuweza kuwa jaili na kuwatunza watu wenye ulemavu pamoja na watoto kwa mchango wao wa hali na mali.
Hata hivyo Henry ametaja changamo zinazowakabili kuwa ni pamoja na shule kwa ajili ya elimu jumuishi.
Kwa upande Naibu meya wa jiji la Tanga Mzamini Shemdoe amewataka viongozi wote pamoja na madiwani waliohudhuria saemina hiyo wazingatie mafunzo hayo ambayo wameyapata na kuchukua hatua ili kujibu changamoto ambayo wameelezwa na kituo hicho.

No comments:

Post a Comment