BOBAN AKANA KULIPWA MSHAHARA NA DIAMOND PLUTNUMZZ
Maestro midfield wa zamani wa Simba SC,
Haruna Moshi ‘Boban’, amekanusha vikali taarifa zilizoibuka hivi karibuni za
kulipwa mshahara na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ baada ya
kutua kwenye timu ya Friends Rangers inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza.
Hivi
karibuni, vyombo mbalimbali vya habari viliripoti taarifa za msanii huyo
kujitolea kumlipa mashahara kiungo mshambuliaji huyo aliyetesa akiwa Simba Sh
400,000 kwa mwezi.
Boban alisema kuwa anashangaa kusikia
taarifa hizo na hajui zimetokea wapi na kuwataka watu kujua kwamba hazina
ukweli hata kidogo.
Madinda aliyefariki dunia
ghafla Jumatano wiki hii, alizikwa jana baada ya kuwa Polisi imetoa mwili wake
baada ya juzi kuzuia maziko yake ili kwanza kufanyia uchunguzi mwili huo
kutokana na kifo hicho kisicho cha kawaida cha mnenguaji huyo aliyejipatia
umaarufu mkubwa nchini.Msanii huyo ambaye katika siku za mwisho alijiunga na bendi ya Extra Bongo chini ya uongozi wa Ali Choki, kifo chake kinaaminika kuwa kimesababishwa na matumizi ya dawa za kulevya, na siku ya kifo chake, alikutwa hajitambui akiwa barazani kwenye nyumba ya rafiki yake aliyetambuliwa kwa jina la Samira Saleh, eneo la Mabibo katika Manispaa ya Kinondoni.
Choki pamoja na aliyewahi kuwa bosi wake, Asha Baraka mmiliki wa Twanga Pepeta, walikuwa miongoni mwa maelfu ya waombolezaji walioshiriki maziko hayo kuanzia mwili wake ulipowasili nyumbani kwao Mikwambe, Kigamboni.

No comments:
Post a Comment