HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 16 December 2014

"UTITIRI WA MADHEHEBU NA MAKANISA MAPYA NCHINI" WACHUNGAJI TANGA WASEMA SIO MPANGO WA MUNGU..!!



Waandishi: Rebeca Duwe Na Daniel Shemjawa ,TANGA.
Kutokana na kasi ya ongezeko la makanisa hapa nchini baadhi ya Wachungaji wa makanisa mbalimbali jijini Tanga wameeleza wasawasi wao na kusema kuwa utitiri wa madhehebu kwa sasa sio mpango wa Mungu bali upotevu wa utimilifu wa imani.

Wakizungamza na Mtandao huu kwa nyakati tofauti wachungaji hao walikuwa na haya ya kusema 
Mch.kiongozi wa kanisa la  kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Mlingano wilayani Muheza mkoani Tanga Mch.Samweli Mteri alisema  kasi ya ongezeko la madhehebu ya makanisa mbalimbali imeonekana kuwa sio mpango wa Mungu bali ni nguvu za shetani .
Aidha alisema watumishi wanapaswa kuatambua nyakati na majira na kuacha tamaa ya fedha na badala yake wamtumikie Mungu kama neno lilivyosema hubirini injiili ulimwenguni mwote na  kwa kilia kiumbe na wala sio kwa ajili ya maslahii yao binafsi.

Hata hivyo alisema wakristo waache  tabia ya kuhangaika kwa kutafuta miujiza kwa watu  nguvu za giza huku wqakitaja jina la yesu na badala yake waamue wenyewe  kumwomba Mungu ili awajibu mahitaji yao.
Sambamba na hayo Mch.Mteri alitoa wito kwa viongozi wa makanisa kuipa kipaumbele mafundisho ya neno la Mungu kwa vingozi waliochini yao husasani wainjilisti, waalimu wa mitaa na wazee wa makanisa ili wasiibuke  kuwa chanzo cha kuanzisha Madhehebu bali wafundishwe jinsi ya kusimama na kuitetea imani ya kumtumikia Mungu katika Roho na kweli.
Kwa uapande wake Mch..Ernest Kangajaka wa Kanisa la Jerusalem Spiritual Transformation Church (J S T C) lililopo jijini Tanga aliwataka wakristo kuchukua tahadhari na kuacha tabia ya kuhamahama makanisa na badala yake watulie mbele za Mungu wao na kutafuta uso wa Mungu kwani Mungu humsikliza mtu yule ambaye anaomba katika kweli bila ya wasiwasi.

Kangajaka yeye alieleza msimamo wake kuhusu kasi ya kuongezeka kwa makanisa kuwa makanisa yaendelee kuongezeka ila tupime roho zile ambao zinafanya kazi ndani hayo makanisa kwani manabii wameongezeka kwa kasi kubwa katika ulimwengu wa sasa kama ambavyo    Yesu alivyotabiri kuwa nyakati za mwisho kutakuwa na manabii wa uongo na wapinga kristo.

Hata hivyo alisema Waanzilishi wa makanisa wale ambao wanaijua msingi wa imani yao  wachukue watua ya kuwaonya wale ambao hawaendi kwa utaratibu nadani ya makanisa yao ili kusudi jina la Mungu lisiaibike kwani kupitia baadhi ya wachunagaji au  manabii waliojitokeza, jina la Mungu limetukanwa kwa matendo maovu yaliyofanyika kupitia huduma yao.

Alitolea mfano wa watu wanaomwabudu Mungu wa Eliya kuwa ni uongo kwani Mungu ni mmoja tu aliyeumba mbingu na nchi hivyo ni jukumu la klia mkristo kutambua ni roho gani inayomwongoza ili asipotee kwa injli ya uongo bali atafute ni wapi roho yake itapona .
Naye Mch.Ishmael Ngoda wa kanisa la kilutheri la kiinjili Tnazania (KKKT) Usharika wa Kisosora jijini Tanga alisema kuna haja kubwa ya wakristo kutambua nyakati tulionayo ni aina gani hivyo kutokana na kasi ya ongezeko la madhehebu ni jukumu letu sote kutambua kuwa tunaelekea wapi au tunaenda wapi "alisema".

No comments:

Post a Comment