HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 16 December 2014

HIZI NDIZO SABABU ZA KITUO CHA AFYA PONGWE KUPEWA TUZO..!!


Na Rebeca Duwe.TANGA
WIZARA ya afya na Ustawi wa Jamii imetoa tunzo ya BIMOC kwa Kituo cha afya cha Pongwe pamoja na vyeti maalum vya daraja la kwanza. 
Hatua hii imekuja baada ya kuridhika na  huduma bora  ya dharura kwa wanawake wajawazito na watoto inayotolewa na kituo hicho.

Akifafanua maana ya BIMOC katika hafla fupi iliyofanyika kituoni hapo hii leo mganga mkuu Faisal Ally, mara baada ya kupokea tunzo hiyo amesema hiyo ni kuonyesha kuwa kituo hicho ni bora kwa huduma ya mama na mtoto

Sanjari na hayo pia Mganga huyo ameelezea uwezo mwingine walionao kituoni hapo kama vile kufanya upasuaji, kutoa dawa za usingizi, huduma ya kutoa na kuhifadhi damu salama ambayo wanategemea kuianza hivi karibuni baada ya kukamilika kwa mahitaji ya vifaa kadhaa.

Hata hivyo changamoto inayowakumba katika kutoa huduma kwa mama wajawazito ambayo hutolowa bure ameelezea kuwa ni urejeshaji wa matumizi wanayotumia kuwahudumia.

No comments:

Post a Comment