HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 16 December 2014

MWINGEREZA ABURUZWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUWALAWITI WATOTO WA MITAANI KENYA..!!



Mwalimu wa shule ya umma nchini Uingereza amepatikana na hatia ya kuwalawiti watoto wanaorandaranda mitaani nchini Kenya.Simon Harris alipatikana na hatia ya makosa saba, ikiwemo kuwadhulumu kingono watoto hao katika mji wa Gilgil.


Alipatikana na hatia katika mahakama ya Birmingham kwa makosa manne ya kumiliki picha chafu zinazoonyesha uchi wa waoto wadogo.

Simon Harris
Hata hivyo mahakama haikumpata na hatia ya kitendo cha kuwabaka watoto hao.Haris alikuwa anakabiliwa na maskosa 23 ikiwemo madai 18 ya kuwadhulumu watoto.
Unyama huo ulitendwa wakati Harris alipokuwa anaendesha shirika la kijamii la kuwasaidia watu mapema mwaka wa 1990.Wakati kesi yake ilipokua inaendelea, wendesha mashitaka walisema kuwa aliwahadaa watoto hao wavulana kwenda nye nyumbani kwake iliyojulikana kama "The Green House", kwa kuwapa chakula na kuwapa hifadhi.

Kabla ya kesi hio kuanza, Harris alikiri makosa sita ya kuwadhuru watoto hao waliokuwa kati ya umri wa miaka 13-14 alipokuwa bado mwalimu wa chuo cha Davon.
Awali alikuwa anakabiliwa na makosa 22 kuhusiana na dhuluma hizo alizozitenda nchini Kenya lakini jaji Philip Parker QC alisema kuwa makosa manne dhidi ya mtuhumiwa yaliodnolewa wakati kesi hio ilipokuwa inasikilizwa.

No comments:

Post a Comment