HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 10 December 2014

TANGA BADO NJIA MUHIMU YA WAHAMIAJI HARAMU "18 WAKAMATWA"



Matukio ya kumatwa kwa Wahamiaji Mkoani Tanga yamezidi kushamiri ambapo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Ally Mbukuzi mwenye umri wa miaka 17 mkulima na mkazi wa Putini kata ya Chongoleani Wilaya ya Tanga kwa kosa la kuwaasafirisha wahamiaji haramu wapatao sita (6) ambao ni Raia wa Ethiopia.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga Frasser Kashai amesema kuwa mnamo tarehe 8 Disemba mwaka huu majira ya saa saba 13:00 mchana, huko katika  kisiwa cha Jambe Kata ya Tongoni Tarafa ya Pongwe Wilaya Tanga wamekamatwa wahamiaji hao ambao wametambulika kwa majina ya Dolec Dalalo umri wa miaka 28, Alaleus  Tesame umri wa miaka 21, Hashinavia Shamibu umri wa miaka 23, Taken Ndasalh umri wa miaka 20,Tamesgen Kisfon umri wa miaka 20, Mihon Eriamin umri wa miaka 22.
Aidha mtuhumiwa amekiri kufanya kufanya biashara hiyo ya usafirishaji wa wahamiaji haramu hivyo atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi wa awali kukamilika.

Katika tukio jingine Gari yenye namba za usajili T.131 AZZ SCANIA mali ya kampuni ya Saibaba limekamatwa likiwa na  Raia 12 wa  Ethiopia likiwasafirisha kutokea Arusha kuelekea jijini Dar es salaam
Raia hao wamekamatwa majira ya saa 10:30 jioni maeneo ya Mbwiko Kata ya Mbwiko Tarafa ya Mombo barabara kuu ya Mombo –Segera Wilayani Korogwe.

Kamanda kashai amewataja Raia hao kuwa ni Kashoma Bayen umri wa miaka 24,Berchano Gamada umri wa miaka 32, Awal Jamal  umri wa miaka 23  ,Yanis Gatiso umri wa miaka 28, Metson Sipril  umri wa miaka 21,Tashona Hayalis umri wa miaka 30.
Wengine ni Adino Samiru umri wa miaka 20, Kengeny  Siyun umri wa miak 22 ,Charnes Egesa umri wa miaka 20, Abdi Bandru umri wa miaka 21, Siumanda Siumanda umri wa miaka 26 na Na Malako Abuu umri wa miaka 23.
Watuhumiwa wote wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayowakabili pale upepelezi wa awali utakapo kamilika.

No comments:

Post a Comment