HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 11 December 2014

MICHEZO:COASTAL UNION YAMSAJILI IBRAHIM HUMUD ALIYEKUWA SIMBA.!



Na Godwin Henry .TANGA
ALIYEKUWA kiungo wa Sofapaka ya Kenya, Abdulhalim Humud amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea timu ya Coastal Union ya Tanga yenye maskani yake Barabara ya 11 mjini hapa.

Humud, ambaye aliwahi kuzichezea klabu mbalimbali hapa nchini zikiwemo Simba, Mtibwa na Azam, amehaidi kufanya makubwa kwenye kikosi cha wagosi wa kaya ambacho kinajiwinda na michuano ya Ligi Kuu Tanzania bara.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Ofisa habari wa Coastal Union, Oscar Assenga alisema kuwa wana matumaini makubwa na mchezaji huyo ambaye alikuwa tishio kwenye klabu alizowahi kuchezea nchini.Kwa mujibu wa Assenga, Humud tayari ameshatua jijini Tanga na ameungana na wachezaji wenzake kwenye mazoezi yanayoendelea kwenye viwanja wa Disuza chini ya Mkurugenzi wa benchi la ufundi la Coastal Union, Mohamed Kampira.

Wachezaji wengine waliosajiliwa kwenye dirisha dogo ni Bakari Sadiq kutoka Friends Rangers ya Dar es Salaam, Godfrey Wambura ambaye alikuwa mchezaji wa Kagera Sugar.Kwa upande wake Humud, alisema amejisikia faraja kubwa kusajiliwa na Coastal Union na kuahidi kushirikiana na wachezaji wengine ili kuipa mafanikio timu hiyo.

Wakati huo huo, klabu hiyo imeingia mkataba wa mwaka mmoja na aliyekuwa kocha wa makipa wa Yanga, Mfaume Athumani kuwanoa makipa wa kikosi hicho.

Assenga alisema kocha huyo anachukua mikoba ya Razack Siwa aliyewahi kuwanoa makipa wa timu hiyo kabla ya kuondoka.Assenga alisema kocha huyo aliwahi kuzifundisha timu za soka Yanga, Ashanti United na Timu ya Taifa ya Vijana U-20, hivyo wana matumaini makubwa ataimarisha safu ya walinda milango kwenye kikosi hicho na kuipa mafanikio.

No comments:

Post a Comment