HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 4 December 2014

NI AJABU NA KWELI BINTI ALIEONGOZA UFAULU DARASA LA SABA AOZESHWA BABU WA MIAKA 50 KWA MAHARI YA SUKARI KILO MBILI.



Mmoja wa wanafunzi walioongoza mtihani wa Taifa wa darasa la saba mwaka huu mwenye umri wa miaka 16 kutoka wilayani Siha Mkoani Kilimanjaro anadaiwa kuozwa kwa mwanaume mwenye umri wa miaka 50 baada ya wazazi wake kupewa sukari kilo mbili kama mahari.

Kutokana na hali hiyo, Mtandao wa Kuelimisha Jamii kuhusu Ukeketaji mkoani Kilimanjaro (NAFGEM), umefanya jitihada za kumuokoa pamoja na wanafunzi wa kike wengine 15 waliotaka kufanyiwa vitendo vya ukeketaji kwa ngariba.

Msichana huyo wa miaka 16 wa kabila la kimasai kutoka kata ya Orkolili (jina limehifadhiwa) baada ya kufaulu mtihani huo, aliozeshwa kwa mmoja wa wanaume ambaye ni wafugaji wa kabila hilo.
Meneja Mipango wa Mtandao wa Kuelimisha Jamii kuhusu Ukeketeaji mkoani Kilimanjaro (NAFGEM), Honoratha Nasua, alitoa taarifa za kuokolewa kwa wanafunzi hao katika kijiji cha Naibili wilayani hapa.

“Wanafunzi 15 walikuwa wameandaliwa kwa ajili ya kukeketwa wakati wa mapumziko ya mwezi Desemba, mwaka huu na waliamriwa kuacha shule ili waozeshwe baada ya kukeketwa,” alisema.
Nasua alisema katika utafiti huo wamefanikiwa kupata orodha ya Mangariba wanaohusika katika mtandao wa ukeketaji.Alisema suala la mwanafunzi huyo aliyeozeshwa limefikishwa katika Dawati la Jinsia la Polisi Wilaya ya Siha mkoani humo kwa ajili ya kuchukua hatua zaidi za kisheria.

Kwa upande wake, Mkuu wa Dawati la Ukatili wa Kijinsia mkoa wa Kilimanjaro, Grace Lyimo, alisema mwanafunzi huyo aliyeozeshwa aliokolewa baada ya polisi na maofisa wa NAFGEM kuingilia kati.
Alisema wazazi wa wanafunzi huyo wameshiriki kudidimiza maendeleo ya mtoto wao kwa kukubali aolewe na kubuni mbinu mpya ya kukeketa watoto wachanga ili kukwepa vyombo vya dola na mkono wa wanaharakati.

Chanzo: Nipashe

No comments:

Post a Comment