HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 11 December 2014

MSICHANA WA KAZI ALIYETESA MTOTO AKIRI MAKOSA, SASA KUHUKUMIWA JUMATANO DESEMBA 11, 2014



Msichana wa kazi aliyetikisa vyombo vya habari duniani kwa kumtesa mtoto wa miezi 18, Arnella Kamanz aliyekuwa kwenye uangalizi wake huko Uganda, amekiri makosa mbele ya mahaka nchini humo.


Tumuhiirwe
Jolly Tumuhiirwe, mwenye umri wa miaka 22, alifanya ukatili uliochukiwa na watu wote Duniani, ambapo alinaswa na camera ya siri, akimtandika mtoto wa mdosi wake kwa kumkanyaga mgongoni akiwa ameanguka chini, kumchapa na kitu kisichojulikana na kumpiga mateke na makofi ya nguvu usoni.
Kitendo hicho kilifuatia mtoto huyo wa kike, kushindwa kula, kutokana na kasi ya ulishwaji ambapo Tumuhiirwe, alikuwa akimlisha mtoto huyo kwa kasi ya ajabu, kwa kushindilia vijiko mdomoni mfululizo.
Rnella Kamanzi,
Binti mwenye umri wa miezi 18 tu,
aliyeteswa na Tumuhiirwe

Huenda mahakama hiyo ikamuhukumu kifungo cha hadi miaka 15 jela, kulipa faini au vyote kwa pamoja. Msichana huyo katika maelezo yake mahakamani, aliomba radhi wazazi wa mtoto huyo, taifa la uganda na walimwengu wote waliokereka na kitendo chake na kuomba msamaha. 

Hukumu yake itatolewa Jumatano Desemba 11, 2014.

Hata hivyo wakili wa msichana huyo wa kazi aliyekiri kosa hilo Desemba 8, 2014, amedai kuwa mteja wake hakutendewa haki kwa vile hakuelewa mashtaka yaliyokuwa yakimkabili.

No comments:

Post a Comment