HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 5 December 2014

MICHEZO:NYOSSO ATUA MBEYA CITY, SIMBA YAKWAMA KWA MARWANDA..!!




SIMBA, MTIBWA ZAFIKIA ASILIMIA 90 ILI KESSY ATUE ZAKE MSIMBAZI
Uongozi wa Klabu ya Simba umefunguka kuwa, upo katika hatua za mwisho za kumalizana na beki namba mbili wa Mtibwa Sugar, Hamis Kessy licha ya kuripotiwa kuwepo kwa ugumu wa mchakato huo wa usajili.
Hata hivyo kumekuwa na taarifa kwamba mazungumzo yako katika hatua nzuri sana na pande zote mbili, yaani Simba na Mtibwa Sugar zimekubali kwamba zimefanya mazungumzo.
Simba ambayo imeshampa mkapata wa miaka mwili raia huyo wa Uganda, imekuwa katika mazungumzo ya kumsajili Kessy licha ya kuwa Mtibwa imekuwa ikiweka ngumu, kuna uwezekano wa kukubali kutokana na mchezaji mwenyewe kuonyesha nia ya kukubali dili.


Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, alifunguka kuwa mazungumzo yanaendelea vizuri na kama kila kitu kitaenda vizuri, kuna uwezekano wa usajili huo kukamilika ndani ya siku chache zijazo.
Mkurugenzi wa Mtibwa Sugar, Jamal Bayser, alisema ni kweli mazungumzo yanaendelea.
Wakati huohuo, mchakato wa Simba kumuwania beki mwingine wa timu hiyo, Salim Mbonde, umeendelea lakini dalili zinaonyesha kuwa Mtibwa imegoma katakata kumuuza mchezaji huyo.

Taarifa kutoka Mtibwa zinaeleza kuwa klabu hiyo inahofia kuuza wachezaji wake muhimu kwa kuwa ligi bado inaendelea, hivyo suala la kumuuza mchezaji huyo kwa sasa wamelifuta rasmi.

Uongozi wa Simba umechukua uamuzi wa kusitisha kumsajili mshambuliaji Danny Mrwanda wa Polisi Morogoro.

Simba imefikia uamuzi huo baada ya kugundua hakusema ukweli kuhusiana na mkataba wake na Polisi Morogoro.
Habari za uhakika zimeeleza, Mrwanda hakuiambia Simba kama mkataba wake unamzuia kusaini hapa nchini lakini unamruhusu kwenda nje ya Tanzania bila ya kipingamizi.

Mlinzi wa kati Juma Nyosso amejiunga na kikosi cha Mbeya City Fc kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Akizungumza mara baada ya kuisaini mkataba  huo kwenye  ofisi za timu zilizopo jengo la Mkapa Hall jijini Mbeya,  Nyoso aliyewahi kucheza kwenye timu za Ashanti United, Simba na Coastal Union, alisema  amekubari kujiunga na City kwa mkataba wa mwaka mmoja kwa imani kuwa utatosha  kuushawishi uongozi wa timu kumpa mkataba mrefu zaidi mara baada ya huu wa sasa.

Akiendelea zaidi beki huyo aliyewahi pia kucheza  kwenye kikosi cha timu ya Taifa  ‘Taifa Stars’ alisema kuwa  mafanikio iliyopata Mbeya City msimu uliopita yamekuwa sababu kubwa ya yeye kukubari kujiunga na City huku akiamini kuwa amekuja kuongeza nguvu kwenye timu bora ili kuhakikisha mafanikio ya msimu uliopita yanafanikiwa tena
.Kwa upande wake Katibu Mkuu wa City Emmanuel Kimbe alimshukuru Nyosso kwa kukubari kujiunga na timu hii huku akiamini kuwa uzoefu alionao mchezaji huyo utasaidia kuimarisha safu ya ulinzi kwenye kikosi cha City.Kwa sasa Nyosso tayari yuko na kikosi cha City kilichosafiri kwenda mjini Songea  kwa ajiri ya michezo ya kirafiki.

No comments:

Post a Comment