HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 5 December 2014

MKAAZI WA KANGE AKAMATWA NA POLISI AKIWA NA KILO 1 NA MISOKOTO 7 YA BANGI



Jeshi la Polisi Mkoani Tanga linamshikilia mtu mmoja aliejulikana kwa jina la Saidi Hamisi mmakonde mwenye umri wa miaka 28 mkazi wa Kange Kata ya Maweni, Tarafa ya Pongwe jijini Tanga baada ya kumkamata akiwa na Kilo 1 na misokoto 7 ya mihadarati aina ya Bhangi.

Akithibitisha kukamatwa kwa mtu huyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Fresser Kashai ameuambia mtandao huu kuwa mtuhumiwa amekiri kufanya biashara hiyo ya bhangi kwa lengo la kujipatia kipato.

Kamanda Kashai amesema mtuhumiwa bado anashikiliwa na jeshi la polisi na atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayo mkabili baada ya upelelezi wa awali kukamilika.
Jeshi la Polisi mkoani hapa linatoa wito kwa wakazi wa jiji la Tanga kufanya biashara halali na kuacha kabisa biashara haramu za uuzaji wa madawa yak kulevya kwa sababu yana madhara makubwa mtumiaji na vilevile ni kinyume cha Sheria, na yeyote atakae bainika kujihusisha na Biashara hiyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

No comments:

Post a Comment