HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 10 December 2014

MICHEZO NA BURUDANI: ALY KIBA AFUNGUKIA KOLABO, DIAMOND ATAMBA KUIBEBA TANZANIA.



POGBA KUREJEA MANCHESTER.
Msimu wa usajili unakaribia kufunguliwa mwezi wa kwanza huko Ulaya klabu nyingi za nchi hizo ziko kwenye jitihada za kutaka kuboresha vikosi vyao.
Klabu ya Manchester City imeanza mchakato wa kutaka kumchukua mchezaji kutoka kwenye timu ya Juventus Paul Pogba ili achukue nafasi ya Yaya Toure anayetarajiwa kuondoka kwenye msimu ujao wa usajili.
Paul Pogba alikuwa mchezaji wa klabu ya Manchester United kabla ya kusajiliwa huko Italia kwenye klabu ya Juventus.

WEMA APAMBANA KUPATA MAFANIKIO.
“Mimi siwezi kuringia umaarufu wakati najiona sina mafanikio, nitafanya kila mbinu nipate mafanikio makubwa zaidi, niweze kuijenga heshima ya jina langu kwa mashabiki,” alisema.
Muigizaji Wema Sepetu, amesema mawazo yake yamejikita kutafuta mbinu za kumwezesha kupata mafanikio zaidi.
Amesema dhamira yake, anataka kuwa na mafanikio zaidi ya aliyonayo hivi sasa.
Wema aliyewahi kuwa Miss Tanzania, amesema umaarufu kwake si muhimu kama, ilivyo kwa baadhi ya wasanii wengine nchini.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Wema alisema anashangazwa na baadhi ya wasanii wanaothamini umaarufu kuliko mafanikio.
“Mimi siwezi kuringia umaarufu wakati najiona sina mafanikio, nitafanya kila mbinu nipate mafanikio makubwa zaidi, niweze kuijenga heshima ya jina langu kwa mashabiki,” alisema.
Alisema, mawazo yake ameyaelekeza zaidi kujua namna ya kupata fedha kwani ukifanikiwa, kila jambo huwa rahisi,” alisema Wema.

ALY KIBA AFUNGUKA KUHUSU KOLABO.
“Kufanya ‘kolabo’ na mtu unayemtaka ni maamuzi ya msanii mwenyewe, si kila mtu ajue kama unamshirikisha fulani.
Mkali wa muziki wa miondoko ya kizazi kipya Ali Kiba, amesema hawezi kusema atamshirikisha msanii yupi baada ya kuachia kibao cha ‘Mwana.’
Kibao hicho cha Mwana, kimeonekana kufanya vyema, kukubalika katika soko la muziki nchini.
Kiba amesema lengo la kufanya hivyo ni kutaka mambo yake yaende kimya kimya.
Akizungumza na Mwandishi Wetu, Kiba alisema kuna siku, atamshirikisha Naseeb Abdul ‘Diamond’, kuwadhihirishia mashabiki, hakuna bifu kati yao.
Alisema hakuna shabiki, aliyejua kama angefanya nyimbo kwa kumshirikisha mwanamuziki maarufu, Robert Kelly.
Alisema anataka kuendelea na utaratibu wa kufanya mambo kimya kimya, kuwashangaza mashabiki.
Alisema hataki kujisifu, ingawa ukweli uko wazi yeye ni msanii mahiri, anataka kuendelea kudhihirisha hilo.
“Kufanya ‘kolabo’ na mtu unayemtaka ni maamuzi ya msanii mwenyewe, si kila mtu ajue kama unamshirikisha fulani.
“Kuna siku nitamshirikisha Diamond, lengo langu nataka kuwaonyesha watu kwamba hatuna ugomvi,” alisema Kiba.

DIAMOND ATAMBA KUIBEBA TANZANIA
“Ukweli mimi sina muda wa kufanya starehe, ukinikuta nafanya starehe basi ujue hapo kuna fedha natarajia kupata, nauthamini muziki wangu, sitaki niporomoke bado sijatimiza ndoto zangu,” alisema Diamond.

Naseeb Abdul ‘Diamond’ amesema ana kazi moja tu, kuitambulisha Tanzania kimataifa kupitia muziki, hajali wanaomfanyia majungu.
Akizungumza na Mwandishi Wetu Diamond, alisema muziki kwake siyo starehe, anatumia muda mwingi kufikiria na kubuni mambo yenye manufaa kwangu na Taifa kwa ujumla.

Msanii huyo alisema dhamira yake, ni kuona Tanzania inajulikana katika anga za kimataifa, kupitia tungo zake.
Alisema baadhi ya wasanii wamekuwa wakiendekeza starehe zaidi bila kujali kazi matokeo, yake kushindwa kupata mafanikio waliyoyakusudia.
“Ukweli mimi sina muda wa kufanya starehe, ukinikuta nafanya starehe basi ujue hapo kuna fedha natarajia kupata, nauthamini muziki wangu, sitaki niporomoke bado sijatimiza ndoto zangu,” alisema Diamond.
Aliwataka wasanii wezake wasiwe wachoyo, wadumishe upendo ambao utawezesha kupiga hatua kupitia tasnia ya muziki.

No comments:

Post a Comment