HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 9 December 2014

DANA DANA ZA HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA NA STENDI MPYA ILIYOKO KANGE.



WAKAZI wa Jiji la Tanga wametakiwa kukitumia kituo kipya cha mabasi yaendayo mikoani na wilayani kilichopo Kange ingawa
bado kuna baadhi ya changamoto za kukamika kwake.
Rai hiyo ilitolewa na Mstahiki Meya wa Jiji hilo, Omary Gulledy alipozungumza na madiwani katika kikao cha baraza kilichofanyika jijini hapa.


Alisema wakazi wa Tanga wasione kimya katika umaliziwaji wa kituo hicho bali ni serikali inaendelea na mchakato wa kufikisha huduma zote muhimu kwenye stendi hiyo mpya.
Sambamba na hayo Gulledy alisema lengo hasa la kuhamishia stendi hiyo Kange ni kulikuza jiji baada ya kituo cha mabasi kilichokuwepo kuwa kidogo.

Kwa upande wake Naibu Meya wa jiji hilo Mzamini Shemdoe alisema kuna mipango ya muda mfupi na mrefu kwa ajili ya kujenga vibanda vya biashara vya muda ili kukidhi mahitaji ya wasafiri na wakazi kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment