HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 9 December 2014

MIAKA 53 YA UHURU NA ESCROW: WANAFUNZI WA CHUO CHA UALIMU KOROGWE(TANGA) WAANDAMANA KUDAI MIKOPO WALIYOAHIDIWA NA SERIKALI.



Maandamano ya Wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Korogwe yaliyokuwa yakiishinikiza Serikali kutimiza Serikali kutimiza ahadi yake ya kuwapatia mikopo jana yaligonga mwamba baada ya Askari Polisi wenye mabomu ya kutoa machozi kufanikiwa  kuwatawanya waandamanaji hao.
 
Maandamano hayo yalianza majira ya saa tano za Asubuhi ambapo kabla ya hapo waandamanaji waliasisi mgomo wa kutokula chakula chochote wala kuingia  Darasani hadi hapo madai yao ya Msingi yatakapo tekelezwa.


Mmoja wa wandamanaji hao ambaye ni Kiongozi aliyeomba jina lake lihifadhiwe alisema walifikia hatua hiyo baada ya jitihada zao za kuwasiliana na katibu mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundikugonga mwamba.

Amesema wakati wanaomba kujiunga na chuo hicho cha alimu walielezwa kwamba wangepewa mikopo huku wakiahidiwa kupewa upendeleo wa kusoma Diploma ya juu kwa masomo ya Sayansi na hisabati.

Hata hivyo wakati wakiulizia mikopo yao walipigwa mpira huku chuo cha TTC nacho kikiwahimiza kulipa ada ya Sh 600,000/= ili kuweza kuwasajili.

Amesema kuna baadhi yao waliweza kulipa ada hiyo huku wengine wakilipa nusu na robo ili waweze kusajiliwa huku wakiendelea kuwasilisha kilio chao cha kutolipwa mikopo waliyo ahidiwa na katibu Mkuu kupitia Bunge.

Ameendelea kueleza kuwa cha kusikitisha zaidi wamekuwa wakipewa majibu ya kukatisha tamaa wakielezwa kuwa ni siasa zilizojitokeza hivyo wao kujikuta hawana sehemu ya kupata msaada.
“Tumepambana tukiulizia ahadi yetu lakini tumekuwa tukipigwa mpira huku tukipewa majibu yasiyo na tija,tulianza na mgomo wa ndani, ikaja kutokula na kuingia madarasani  na leo tunaandamana” alisema mtoa habari huyo.

Aidha amesema wanafunzi hao wa Ualimu wanahisi kurubuniwakatika mchakato mzima kwani baadhai yao kama wangepewa ukweli mapema wasingeweza kujiunga na chuo hicho kutokana na hali za familia zao kuwa duni.

Naye  Mkuu wa chuo cha Ualimu Korogwe Lyana Mmbaji ameeleza kusikitishwa kwake na maandaano hayo yasiyo rasmi ambapo amesema alilazimika kuvipa taaraifa vyombo vya ulinzi na Usalamaili kutuliza hali ya hewa.

Mmbaji amesema baada ya Polisi kuwatawanya waandamanaji hao mazungumzo yaliyowakutanisha viongozi  wa wanafunzi hao wa mwaka wa kwanza nia viongozi wa Serikali Wilayani Korogwe yamekuwa yakiendelea ambapo bado haijafahamika maazimio.

No comments:

Post a Comment