HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 23 December 2014

MICHEZO: COASTAL UNION YAICHAPA 3-1 KOMBAINI YA MOMBASA "MAANDALIZI LIGI KUU"



Mabingwa wa Tanzania bara wa mwaka 1988, Coastal union wameichapa kombaini ya Mombasa magoli 3-1 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye uwanja wa Mombasa Sport club jana.Katika mchezo huo maalum wa kujianda na mwendelezo wa ligi kuu ya vodacom, kombain ya Mombasa walikuwa wa mwanzo kupata goli kupiti kwa Makame Salim katika dakika ya 15 ya mchezo.

Mkenya Ramadhani Salim aliisawazishia Coastal union katika dakika ya 32 na kupelekea kwenda mapumziko wakiwa sare ya goli 1-1.Katika kipindi cha pili Mkongoman Imbem aliiandikia Coastal union goli la pili katika dakika ya 46 na kurejea tena katika nyavu za kombaini ya Mombasa katika dakika ya 73 kwa mkwaju wa penati.

Mchezo huo ambao ni wa pili kwa kocha James Nyende Nandwa ulimalizika kwa Coastal union kuibuka na ushindi wa goli 3-1.Nandwa amejiunga na Coastal union kuchukwa nafasi ya Yusuf Chippo aliyejiunga na AFC Leopard kama kocha msaidizi.

Mchezo wa kwanza kwa Nandwa ulikuwa ni dhidi ya Mwadui FC inayoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania na mchezo huo ulimalizika kwa sare ya bila kufungana.

No comments:

Post a Comment