HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 19 December 2014

KOCHA ALIYEMNOA VICTOR WANYAMA WA SOUTHAMPTON ATUA COASTAL UNION NA KUAHIDI MAKUBWA.


Aliyekuwa Kocha wa Kiungo mkenya Victor Wanyama anaechezea klabu ya Southampton ya Uingereza James Nandwa ameingia mkataba wa mwaka mmoja na vogogo wa Soka mkoani Tanga COASTAL UNION.

James Nandwa kulia
Kocha huyo anachukua mikoba iliyoachwa na Kocha Yusuph Chippo aliyekwenda nchini kwao Kenya kutokana na matatizo ya kifamilia kuwa kwenye hali ambayo sio nzuri jambo ambalo lilipelekea kushindwa kurudi nchini kwa ajili ya kuendelea kukinoa kikosi hicho.

Akizungumza mara baada ya kutua jijini Tanga jana na kulakiwa na vingozi wa klabu hiyo wakiongozwa na Meneja wao, Akida Machai katibu mkuu pamoja na wajumbe wa kamati ya utendaji, Kocha huyo amesema dhamira yake kubwa ni kuhahakikisha anaipa mafanikio makubwa timu hiyo.

Akizungumza kleo ofisa habari wa klabu hiyo Oscar Senga amesema kuwa ujio wa Kocha huyo utawezesha timu yao kufikia malengo waliyo jiwekea ambayo ni kuhakikisha wanachukua ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.

Kocha Nandwaamesema kuwa kitu cha kwanza ni kuhakikisha timu hiyo inafikia malengo yake ya kuwa timu bora Tanzania na hatimaye ipate nafasi ya kushikiriki michuano ya kimataifa.
Kocha huyo aliwahi kuzifundisha timu za Soka za Harambee Stars,AFC Leopard na Utalii zote za Kenya na kuzipatia mafanikio makubwa.

No comments:

Post a Comment