HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 12 December 2014

BURUDANI: LULU ALIA NA WAANDAAJI WA FILAMU, IDRIS KUSAKA HESHIMA, SHETA APANGA KUWAFURAHISHA MASHABIKI WAKE..!!!



HIKI NI KILIO CHA LULU KWA WATAYARISHAJI FILAMU NCHINI.
Muigizaji Elizabeth Michael a.k.a Lulu amedai kuwa waongozaji na watayarishaji wa filamu wengi ni wale wale, hakuna wapya.
Amesema jambo hilo, linampa hofu kuwepo kwa upendeleo kwa wasanii wapya kuliko, wakongwe.
“Waongozaji a filamu ni wachache, naweza kusema ni wale wale, kila siku wasanii wazuri wanaibuka, wanaonyesha uwezo mkubwa,”alisema Lulu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Lulu ameonyesha hofu kuwa, wasanii wakongwe, akiwemo yeye kukosa nafasi kama ilivyokuwa zamani.

“Waongozaji wa filamu ni wachache, naweza kusema ni wale wale, kila siku wasanii wazuri wanaibuka, wanaonyesha uwezo mkubwa,”alisema
Lulu alisema hiyo ndio moja ya sababu inayofanya wasanii wengi kutengeneza filamu zao wenyewe kama waongozaji, watayarishaji wakuu baada ya kukosa nafasi mara kwa mara.
Hivi karibuni, Lulu alitoa filamu aliyoiandaa mwenyewe ya ‘Mapenzi ya Mungu,’ ambayo amemshirikisha mama wa marehemu, Steven Kanumba.

 KAJALA SASA ATAMBA KWA KIMYA CHAKE KINA MSHINDO.
Muigizaji wa filamu Kajala Masanja akiwa na mwanae Paula.
Muigizaji wa filamu nchini, Kajala Masanja amesema ukimya wake, utaibua kishindo kizito baadae.
Amesema hivi sasa, ameupa kisogo uigizaji, anafanya biashara zingine kwa ajili ya kumuingizia mapato.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kajala alisema kamwe hawezi kuacha uigizaji, licha ya baadhi ya watu kusema ‘amefulia.’
“Bado kuna mambo yangu nafuatilia, siwezi kufanya kazi moja tu, filamu pekee bila shughuli zingine, huwezi kutoka kimaisha,” alisema Kajala.
Aliwataka mashabiki wake, kuwa tayari, anajiandaa kuachia kazi ya kufungia mwaka 2014.
“Wakae mkao wa kula, naandaa kazi nzuri, naamini wataipenda, watakapoiona.”

IDRIS KUSAKAHESHIMA KWANZA, SIYO FEDHA.
“Kwa kweli, sijafurahia fedha kabisa, najivunia heshima niliyopewa na watanzania wenzangu, wameniwezesha kwa kura baada ya kuona nafaa,” alisema Idris Sultan.
Mshindi wa shindano la Big Brother Africa, Idris Sultan amesema hafurahii fedha alizopata, bali heshima aliyopewa na watanzania.

Sultan, aliwabwaga wenzake na kujinyakulia kitita cha dola 300,000 (Zaidi ya sh. milioni 480) baada ya kuishi kwenye jumba la BBA kwa siku 63.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Sultan, alisema kwamba ushindi huo, umedhihirisha namna watanzania wenzake, wanavyompenda na walivyokuwa bega kwa bega naye.
“Kwa kweli, sijafurahia fedha kabisa, najivunia heshima niliyopewa na watanzania wenzangu, wameniwezesha kwa kura baada ya kuona nafaa,” alisema Sultan.
Aidha, Sultan alisema hakutarajia kushinda, kutokana na changamoto zilizokuwepo ndani ya jumba.
“Shindano lilikuwa gumu, watanzania ndiyo wameniwezesha kuibuka mshindi. Wamenipa heshima kubwa,” alisema Sultan.

SHETTA ASEMA MASHABIKI HAWATAFURAHI ASIPOPIGA HATUA.
 “Nchi kama Afrika Kusini ambayo, nimeamua kuwatumia watayarishaji video wa huko, kuna uwezekano mkubwa wa kutengeneza uhusiano wa kimataifa na wasanii wakubwa, sidhani kama wapenzi wangu watafurahi kuniona, niko pale pale, sipigi hatua,” alisema Shetta.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Nurdin Bilal a.k.a Shetta, amesema hadhani kama mashabiki wake, watafurahi kumuona hapigi hatua ya kufanikiwa kimuziki.
Shetta, amesema kutokana na hilo, ndiyo sababu ya kuchanganya vionja vya nchi mbalimbali, anaporekodi video za nyimbo zake.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, msanii huyo, alisema mazingira ya Afrika Kusini, amekuwa akiyatumia kunogesha kazi zake.
Alisema bila kufanya hivyo, mashabiki watashindwa kumuelewa, hivyo amekuwa akijenga uhusiano mzuri wa kimataifa, kwa lengo la kufika mbali.

“Nchi kama Afrika Kusini ambayo, nimeamua kuwatumia watayarishaji video wa huko, kuna uwezekano mkubwa wa kutengeneza uhusiano wa kimataifa na wasanii wakubwa, sidhani kama wapenzi wangu watafurahi kuniona, niko pale pale, sipigi hatua,” alisema.

No comments:

Post a Comment