|
Kamanda wa Polisi mkoa wa TANGA
Kamishna
mwandamizi msaidizi wa Polisi SACP, Frasser Kashai
Akionesha noti
bandia kwa waandishi wa habari.
|
Jeshi la polisi mkoani Tanga linawashikilia watu
watatu kwa kosa la kupatikana noti bandia 112 ambazo ni Dola za kimarekani ambazo kama
zingekuwa ni za halali zina thamani ya dola za kimarekani 11,200 ambazo ni sawa
na milioni 20 kwa fedha za kitanzania .
Watuhumiwa hao
Julius Kanza 30 mkazi wa Ubongo, Kenedy Binaga 35 mkazi wa Sinza, na Ramadhani
Saddy 33 mkazi wa Mwenge walikamatwa wakiwa na gari yenye
Chasis namba JLg 100037726.
Akizungumza na
wandishi wa habari kamanda wa Jeshi la
Polisi mkoani hapa, Kamishna mwandamizi msaidizi SACP, Frasser Kashai kuhusiana na tukio hilo amesema limetokea
Novemba 17 mwaka huu majira ya sa 7:30 mchana
maeneo ya barabara ya 16 Kata na Tarafa ya Ngamiani Kati Wilayani Tanga.
Aidha watuhumiwa
hao wamekiri kufanya biashara hiyo ya uuzaji wa fedha bandia. Wote wamekamatwa
na watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinayo wakabili baada ya upelelezi wa
awali kukamilika.
Kamanda Kashai alisema kuwa tukio hilo la mauaji hayo lilitokea Novemba 18 mwaka huu majira ya saa kumi na moja na dakika arobaini na tano katika eneo la kijiji cha Vyadigwa Kata ya Kimbe wilayani humo.
Akizungumzia tukio hilo,Kamanda Kashai alisema mkulima wa Vyadigwa alikutwa porini akiwa amejeruhiwa maeneo ya utosini kwa kitu chenye ncha kali na watu wasiojulikana hali iliyomsababishia kifo chake.
Alisema kuwa mkulima huyo alifariki dunia saa kumi jioni wakati akiwakwenye hospitali Teule ya wilaya ya Kilindi (KKKT) ambapo chanzo cha mauaji hayo bado kinachunguzwa
No comments:
Post a Comment