HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 20 November 2014

WENYE HEKIMA MNAWEZA KUNISAIDIA KUTATUA HILI..!!




Hivi Karibuni nilijikuta ktk wakati mgumu pale nilipoombwa Ushauri na Rafiki Yangu wa Karibu ambaye alinisimulia mkasa huu wa kweli ambao unamkuta na bado unamkabili mpaka sasa.

Anaye mpenzi ambaye walikutana zaidi ya miezi mitano sasa, kabla ya kuanzisha mahusiano kila mmoja alikuwa na yake ya kumshawishi mwenzie ambapo yeye alimweleza BINTI kuwa anampenda kwa dhati na hakuwa na mpenzi kwa wakati huo, lakini hakusita kumueleza ukweli kuhusu hali yake ya kuichumi kuwa hana pesa sana ila anajimudu kwa mahitaji ya maisha na hata vingine vidogo vya starehe, binti nae akasema hana Mpenzi kwani alitendwa mara kadha hivyo akaona bora ajiweke pembenia na Mapenzi ili kumsubiri alie chaguo lake na zaidi akamhakikishia kuwa anampenda, hajali pesa na angependa amkute analala chini ili wanze pamoja ujenzi wa familia kwani wote wana lengo la kuonana baadae.

Anapoeshi BEST yangu ni mbali na BINTI kwani ni mkoa mmoja kwa mwingine, kama ilivyo vijana hupenda kusalia nyumbani na wazazi mpaka pale apatapo mwenza au mtu wa kumshawishi kuwakimbia wazazi, hivyo BEST alikuwa bado anaishi na wazazi.
BINTI akawa anamtembelea kwa vipindi kadhaa huku Mapenzi yakinoga kiasi wakafikia hatua nzuri ya uchumba rasmi ambapo binti alitambulishwa kwa wazazi wa BEST.

BEST hakuishia hapo akahakikisha anafanikisha barua ya uchumba na hatima akafahamishwa wa wakweze kuwa amekubaliwa na mahari pia akatajiwa, hivyo mipango ya kuitafuta ikaanza.
Kufikia hapo BINTI akawa anamshawishi BEST atoke kwa wazazi ili anapomtembelea afikie kwake, wazo ambalo BEST alilipokea na kulitekeleza, sasa akapanga chumba.

Lakini wakati huohuo anapaswa kutafuta mahari, gharama za harusi, gharama za kodi ya pango kila mwezi, umeme na maji matumizi yake yeye n.k
Lakini BINTI nae akaibuka na jipya kuwa anahitaji kutumiwa pesa ya matumizi, tena BEST awe anatuma pasipo kuombwa jambo ambalo alilipokea na kuanza kutekeleza japo kwa 50% hakumudu kwani alipoombwa 10000 alituma 5000.
Migongano isiyokuwa na msingi ikaibuka na hata kufikia hatua kuhatarisha mahusiano yao.Kwa kuwa BEST amependa aliamua kuwa mpole kwa kila kitu ili asimkose ampendae, akawa ni wakuomba msamaha na kujishusha kila mara pale wanapokosana.
Sasa imekuwa Mateso na Maumivu kwani Mapenzi yamepungua sana, BEST ameacha kuongea na watu wote usiku ili aongee na binti lakini akimpigia simu BINTI hana cha kuongea, mchana anapiga BINTI anajibu majibu ya mkato, maneno kama bby, honey, “I mic u”,mchumba yamesahaulika, Wakati hapo kabla simu zilikuwa zinagongana hewani kila mmoja nampigia mwenzie, wanakaribishana kula, kila sms haikosi neno bby au kuishia na I LOVE U,
Ule utani wa Wapenzi umekufa na cha kusikitisha BINTI hana mpango wa kumtembelea BEST kwa muda sasa kwa madai yuko bize.Mbaya zaidi binti anamdharau, hamjali na kama Best asipopiga simu BINTI hata kubeep hajaribu.Lakini bado BEST anapenda zaidi na zaidi. *Nimejaribu kutafakari kuwa huenda Pesa ni tatizo lakini bado sijapata jibu la uhakika*

SASA BEST AMEKONDA KWA MAWAZO, NIKIMTAZAMA NI KAMA ANAUMWA..!
AMEKUJA ANAOMBA NIMSHAURI JE.! WAUNGWANA NIANZIE WAPI.????

No comments:

Post a Comment