HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 18 November 2014

BADALA YA KUWASHANGAA WEZI WA PESA PINDA AWASHANGAA WAHISANI..!!



Waziri Mkuu Mizengo Pinda (pichani), amesema kuwa amesononeshwa na uamuzi wa wahisani kuikatia Serikali misaada ya sh trilioni moja kutokana na kashfa ya IPTL.
Pinda, alisema Serikali iko tayari kuwawajibisha watu wawili au zaidi watakaotajwa kuhusika kwenye kashfa ya kuchota fedha kwenye Akaunti Maalum ya Tegeta Escrow, zaidi ya sh bilioni 200, zilizohifadhiwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), lakini hakubaliani na uamuzi wa kukata misaada, kwani unaathiri watu wengi nchini.

Waziri Mkuu Pinda, alitoa kauli hiyo , akijibu maswali ya papo kwa papo wakati wa kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu bungeni.
Pinda, alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk Mohamed (CUF), aliyetaka kujua sababu ya wahisani kukata misaada yao nchini na tamko la Serikali kuhusu hali hiyo.

Akitoa ufafanuzi zaidi wa swali hilo, Pinda alikiri wahisani wamekata misaada yao nchini na mara nyingi wamekuwa na sababu zao mbalimbali, lakini safari hii hatua hiyo imetokana na kashfa ya IPTL.
“Hawa wahisani mara nyingi wamekuwa na sababu mbalimbali na hata huko nyuma walishawahi kufanya hivyo, lakini safari hii wanasema wamekata misaada yao kutokana na kashfa ya IPTL na wanasema wanasubiri ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ije, hili ni jambo linalonisononesha sana kwa sababu uamuzi huo utaathiri watu wengi,” alisema Pinda.

Akitoa msimamo wa Serikali kuhusu kashfa hiyo inayotikisa taifa, Waziri Mkuu Pinda alisema bado hajakabidhiwa ripoti ya CAG na atakapoipokea, hatakuwa na sababu ya kutoileta bungeni.

“Juzi nilimsikia Waziri Lukuvi akisema Serikali haijaipata ripoti ya CAG. Kauli hiyo ni kweli kabisa na nitakapoipata, sina sababu ya kukaa nayo,” alisema Pinda.
Hata hivyo tayari Kamati ya Uongozi ya Bunge, imeagiza ripoti ya CAG ijadiliwe katika mkutano huu wa Bunge Novemba 27 na 28 mwaka huu.
CHANZO:TANZANIA TODAY

No comments:

Post a Comment