HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 18 November 2014

KKKT USHARIKA WA KABUKU WAOMBA MSAADA KUMALIZIA UJENZI WA KANISA JIPYA.



Waamini wakisafisha Eneo la Kanisa Jipya
Na Daniel Raphael. HANDENI
Mwinjilisti wa Kanisa la  Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT Usharika wa Kabuku Raphael Shemjawa amewaomba wadau mbalimbali na mashirika binafsi kujitoa kwa hali na mali kuwasaidia katika ujenzi wa Kanisa jipya unaondelea ushirikani hapo.

Kanisa linalotumika kwa sasa
Shemjawa aliyasema hayo wakati akizungumza na Upendo ofisini kwake hivi karibuni ambapo ameongezea  kwakusema  kuwa  imekuwa ni muda mrefu tangu ujenzi wa kanisa hili ulipo anza mnamo mwaka 2004 hadi sasa ambapo bado ujenzi huo unaonekana kuzolota kwa kukosa msaada.’’Jengo hili nikubwa sana na linahitaji kiasi kikubwa  cha fedha na tukisema tutegemee washarika tu itachukuwa muda hadi kukamilika.Alisema shemjawa.’’

Aidha alisema kuwa kwa sasa jengo wanalo tumia ni dogo sana na limechoka kwakuwa limejengwa muda mrefu  mnamo mwaka 1984 kwa miti na limekuwa likifanyiwa ukarabati mara kwa mara jambo ambalo amesema bado halijakuwa katika hali yakuridhisha nakusema inafikia wakati washarika wanasali nje kwa udogo wakanisa hilo. 
Kanisa jipya


Sambamba  na hayo mwinjilisti huyo pia amewashukuru washarika kwakujitoa marakwamara katika shughuli za ujenzi wa kanisa hilo nakuwataka kuwa na moyo huo huo wakujitoa katika shughuli za kumtumikia Mungu nakusema Mungu atawabariki katika maisha nashughuli zao za kila siku.

No comments:

Post a Comment