HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 18 November 2014

PATA HABARI ZA USAJILI NA HALI ZA WACHEZAJI MAJUU. "clik hapa"



MODRIC NJE MIEZI MITATU.
SHIRIKISHO la Soka la Croatia limethibitisha kuwa majeruhi aliyopata kiungo wa Real Madrid Luka Modric yatamuweka nje ya uwanja mpaka Februari mwakani. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 alipata majeruhi hayo katika kipindi cha kwanza cha mchezo wa kufuzu michuano ya Ulaya mwaka 2016 kati ya Italia na Croatia mbao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1. Modric alitolewa nje na kwenda kufanyiwa vipimo jijini Madrid ambapo majibu yake yameonyesha atakaa nje kwa muda wa miezi mitatu.

Katika taarifa yake shirikisho hilo lilidai kuwa nyota huyo hatahitaji upasuaji kwani tatizo lake litakwisha kwa matibabu ya kawaida. Modric sasa anatarajiwa kukosa michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia itakayofanyika nchini Morocco mwezi ujao.
NURI SAHIN NJIANI KUREJEA UWANJANI.
KIUNGO mahiri wa klabu ya Borussia Dortmund, Nuri Sahin amethibitisha mwenyewe kuwa fiti kwa ajili ya kurejea uwanjani baada ya kupona majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua. Nyota huyo wa kimataifa wa uturuki alikosa maandalizi yote ya msimu kabla ya kufanyiwa upasuaji kufuatia matatizo ya goti huku mchezo wake wa mwisho wa mashindano ukiwa wa fainali ya Kombe la Ujerumani Mei mwaka huu.

Hata hivyo, Sahin mwenye umri wa miaka 26 sasa anakaribia mwishoni kupona huku akikiri hasikii maumivu yeyote na anahitaji kurejea uwanjani haraka iwezekanavyo. Sahin aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii kuwa anatamani kurejea tena uwanjani baada ya maumivu aliyokuwa akisikia kuondoka.KOLN

YAKANUSHA KUMTAKA PODOLSKI.
KLABU ya Koln imekanusha tetesi za kutaka kumsajili mshambuliaji wa Arsenal, Lukas Podolski. Podolski mwenye umri wa miaka 29 ameanza katika kikosi cha kwanza mara moja pekee msimu huu katika mchezo wa Kombe la Ligi dhidi ya Southampton Septemba na sasa nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani amebainisha kuwa anataka kuangalia upya mustakabali katika timu hiyo.

Meneja wa Arsenal, Arsenal Wenger ameshasisitiza kuwa hana mpango wa kumuuza Podolski katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo baada ya kuzagaa tetesi kuwa kuna vulabu nchini ujerumani vilikuwa vikimhitaji. Hata hivyo vilabu hivyo ambavyo ni Schalke na Koln zote zimekanusha tetesi hizo zikidai hazina mpango huo kwasababu hawatakuwa na uwezo wa kifedha za kumnunua.

No comments:

Post a Comment