HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 18 November 2014

FILAMU YA ESCROW YAFIKA PATAMU "click hapa"



RIPOTI ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusu sakata la akaunti ya Tegeta Escrow, imeanza kufanyiwa kazi na Bunge na ndani ya siku nane zijazo, umma utajua ukweli wake. Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alikabidhi ripoti hiyo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto, jana bungeni, na kamati imeanza kazi mara moja. Kwa mujibu wa Ndugai, taarifa hiyo ya CAG ina maoni kwa kila hadidu za rejea kama chombo hicho kilipoagiza wakati ilipotoa kazi kwa mkaguzi huyo.

Aliiagiza kamati hiyo ya Zitto iichambue zaidi na kutoa ushauri wake kwa Bunge kwa kuzingatia ushauri wa CAG pamoja na ushahidi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ambayo iliwahoji wahusika wote wa sakata hilo.

Aliitaka kufanya kazi chini ya Kanuni za Nyongeza za Bunge pamoja na ile ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge katika kushughulikia suala hilo linalosubiriwa kwa hamu baada ya mjadala wa muda mrefu nchini.

Ndugai akimwakilisha Spika wa Bunge, Anne Makinda, alimkabidhi Zitto mbele ya baadhi ya wajumbe wake ripoti hiyo pamoja na juzuu nne kubwa (viambatanisho) vya kuhusu ripoti ya sakata hilo.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikabidhi ripoti hiyo kwa Ofisi ya Spika wiki iliyopita, kabla ya jana Ndugai kuikabidhi kwa Kamati ya Zitto anayesaidiwa na Deo Filikunjombe, Mbunge wa Ludewa (CCM).

Akizungumza baada ya kupokea ripoti hiyo, Zitto alisema atazingatia maelekezo ya Spika ili kuhakikisha wanakamilisha kazi na mchakato mwingine wa kibunge uchukue nafasi yake. Aliwaambia wanahabari baadaye kuwa kamati hiyo katika kushughulikia ripoti hiyo, itafanya kazi zake kiuchunguzi, tofauti na inapofanya kazi nyingine.

No comments:

Post a Comment