HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 24 November 2014

LIGI DARAJA LA KWANZA "SPORT YAICHAPA VILLA SQUAD 2-1 MKWAKWANI.




MABAO Mawili yaliyofungwa na Hassani Materema kunako dakika za 18 na 79 yalitosha kuweza kuwapa ushindi timu ya African Sports wa Mabao 2-1 dhidi ya Villa Squad katika mchezo wa Ligi daraja la kwanza uliochezwa jana katika uwanja wa CCM Mkwakwani jiji Tanga.


African Sports ndio ilikuwa ya kwanza kuweza kupata bao lake katika dakika ya 18 ambalo lilifungwa na Hassani Materema baada ya kutokea piga nikupige langoni mwa Villa Squad  kabla ya Villa Squad kusawadisha dakika ya 36 kupitia Omary Masha.

TImu zote zilikwenda mapumziko zikiwa nguvu sawa ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo timu zote ziliingia uwanjani hapo zikiwa na nguvu mpya baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi wa wachezaji wake.

Wakionekana kujipanga vilivyo,African Sports waliweza kuongeza wimbi la mashambulizi langoni mwa Villa Squad na kufanikiwa kuandika bao la pili dakika ya 79 ambalo likifungwa na Hassani Materema.

No comments:

Post a Comment