HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 24 November 2014

JESHI LA POLISI MKOANI TANGA LAKAMATA KILO 221 ZA MIRUNGI.



Kutokana na jitihada zinazo endelea kufanywa za kuzua nakutokomeza matukio ya kiuhalifu zinazofanywa na Jeshi la Polisi Mkoani hapa Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata kilo zipatazo 221kg za madawa ya kulevya aina ya mirungi zikiwa zimehifadhiwa ndani ya frezer .

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa jeshi la polisi mkoani hapa Frasser kashai amesema tukio hilo limetokea maeneo tofauti katika mkoa huu ambapo amesema manamo tar21 novemba mwaka huu majira ya saa 03:00 usiku huko maeneo ya Raskazone Kata ya Central Tarafa ya Ngamiani Kusini Wilaya ya Tanga Mjini nyumbani mwa mtu mmoja alie fahamika kwa jina la Sambia Abdallah 25 almkutwa amehifadhi bunda 130 za sawa na kg 30 za madawa ya kulevya aina ya mirungi.
Hata hivyo kamanda ameendelea kwa kusema  kuwa  mnamo majira ya saa 02 usiku huko maeneo ya barabara ya 8 Kata na Tarafa ya Ngamiani Kati Wilaya ya Tanga  walikamatwa watu wawili mke na mume waliofahamika kwa majina ya Doti Hamisi 46 na Jamila Sadiki 30  wakiwa na bunda zipatazo 91 ambazo niswa na kg 91 wakiwa wamezihifadhi kwenye freezer ndani ya nyumba yao.
Aidha kamanda amesema watuhumiwa wote wamekamatwa na watafikishwa mahakamani kujibu mashtka mara baada ya upelelezi wa awali kukamilika.
Sambamba na hayo Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi wotde kujiepusha na biashara haramu ya uuzaji wa madawa ya kulevya kwakua yana madhara makubwa sana afya  Za watumiaji wa dawa hizo.

Katika tukio lingine mtu mmoja alie fahamika kwa jina la Elibariki  Michael 46mkazi wa Vunila Kilindi amekutwa akiwa amejinyonga kwakutumia kamba ya katani hadi kufa. Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wajeshi la  polisi moani Tanga Fresssar Kashai amesema tukio hilo limetokea mnamo tar 22 novemba mwaka huumajira ya 08: asubuhi.
Hata hivyo kamanda kasha amesema chanzo ah tukio hilo ni kutikana na ugumu wa maisha aliokuwa nao marehemu.

No comments:

Post a Comment