HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 22 November 2014

KWA HABARI ZA KIMICHEZO KUTOKA MAJUU "click hapa"





CITY BADO INA NAFASI YA SKUHINDA TAJI LA LIGI KUU - PELLEGRINI.



MENEJA wa klabu ya Manchester City, Manuel Pellegrini bado ana uhakika wa kutetea taji la Ligi Kuu pamoja na kupitwa kwa alama nane na vinara Chelsea. City ambao watakuwa wenyeji wa Swansea City leo baada ya mapumziko kupisha mechi za kimataifa kumalizika, wamefanikiwa kushinda mechi moja kati ya sita za mashindano yote walizocheza hivi karibuni.
Kiwango cha timu hiyo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya pia imekuwa ya kusuasua huku wakiwa katika hatari ya kushindwa kuvuka hatua ya makundi. Hata hivyo Pellegrini bado amekuwa na imani na kikosi chake kufanya vyema katika ligi ya nyumbani na Ulaya msimu huu.
Pellegrini amesema sasa sio wakati wa kuangalia yaliyotokea nyuma kwani bado kuna mechi nyingi za kucheza katika ligi na Ulaya. Kocha huyo aliongeza kuwa bado kuna mechi 27 hivyo kuna alama zaidi za kupigania hivyo wataona itakavyokuwa mpaka mwishoni mwa msimu.


SAMMER AONGEZWA MIAKA MITATU BAYERN.


KLABU ya Bayern Munich imetangaza kumuongeza mkataba wa miaka mitatu zaidi mkurugenzi wa michezo wa timu hiyo Matthias Sammer ambao utamalizika mwaka 2018.
Sammer ambaye alikuwa mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Ujerumani na kocha, alijiunga na Bayern mwaka 2012 akitokea Shirikisho la Soka la Ujerumani ambako nako alikuwa mkurugenzi wa michezo.
Akihojiwa na wanahabari Sammer amesema miaka miwili na nusu ambayo ameitumikia klabu hiyo imekuwa na mafanikio makubwa kwani walifikia malengo yao mengi waliyojiwekea. 
Toka atue Bayern, Sammer amefanikiwa kuisaidia timu hiyo kushinda taji la Bundesliga katika msimu wa 2013-2014, Kombe la Ligi sambamba na taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya 2013.


WENGER AMUITIA THIERRY HENRY DILI LA UKOCHA ARSENAL

GWIJI wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry anaweza kurejea katika klabu hiyo kwa mara ya tatu, lakini safari hii kama kocha si mchezaji tena, amesema Arsene Wenge.
Henry’ anamaliza Mkataba wake katika klabu ya New York Red Bulls mwezi ujao mwishoni mwa msimu wa Ligi Kuu ya Marekani, MLS na ingawa hajatangaza kama atastaafu, lakini wengi wanaamini utakuwa mwisho wake wa kucheza.

Henry amewahi kusema angependa kuifundisha Arsenal, wakati anachezea klabu hiyo katika miaka yake minane, ambayo alishinda mataji mawili ya Ligi Kuu na kuwa mfungaji bora wa kihistoria wa klabu kabla ya kutimkia Barcelona mwaka 2007.
Alirejea kwa muda kwa mkopo kutoka New York Januari mwaka 2012 na alifunga jumla ya mabao 228 katika klabu hiyo ya Kaskazini mwa London.

No comments:

Post a Comment