HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 14 August 2014

KOICA WIPATIA SHULE YA MSAMBWENI MSAADA WA VIFAA VYA SH MIL 27



Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Msambweni Bi Halima Muya(Kushoto) na Mkurugenzi wa KOICA nchini Tanzania Seung-Beom Kim(Kulia) wakizindua jengo la maabara ya Masomo ya Sayansi shuleni hapo.
Na Evelyn Balozi. TANGA
SHIRIKA la maendeleo la Korea Kusini KOICA limeipatia shule ya sekondari Msambeni Mkoani hapa msaada wa vifaa vya shule vyenye thamani ya zaidi ya shilingi mil 27 ili kusaidia mpango wa matokeo makubwa sasa.

Akikabidhi msaada huo mkurugenzi wa KOICA nchini Tanzania Seung-Beom Kim amesema ili kufikisha maendeleo kwa wananchi serikali ya nchi yoyote duniani ni lazima kuwekeza katika elimu kama ambavyo Korea Kusini imefanya na kuifanya kuwa taifa kubwa licha ya kutokuwa na rasilimali yoyote katika ardhi yao.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo ya mchepuo wa sayansi yenye miaka mitatu sasa, Halima Muya alisema watatumia msaada huo kuwaandaa wanafunzi wanaopitia shuleni hapo ili kuandaa wasomi na walimu wa masomo ya sayansi ambao ni hitaji kubwa kwa taifa.

Alisema nchi haita weza kukabiliana na wimbi la upungufu wa wanasayansi hususani walimu kama hakutachukuliwa hatua za makusudi kwa kuwaandaa tangu mashuleni.

Vifaa vilivyo tolewa ni Kompyuta moja, Printa moja, Projekta moja, vitabu 720 kwa kila kidato kwenye kila somo la sayansi kupewa vitabu 60 pamoja na uingizaji wa umeme kwenye shule hiyo.

Mkurugenzi wa KOICA nchini Tanzania Seung-Beom Kim (aliesimama) akizungumza wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya Misaada kwa Shule ya Sekondari Msambweni jijini Tanga
Aidha KOICA imeboresha chumba cha maabara kwa shule hiyo pamoja na kuwezesha vifaa ikiwemo kemikali za kufanyia mazoezo ya vitendo, kabati la kuhifadhia vifaa vya maabara, viatu vya maabara, meza tatu na viti 60.

Nae kaimu katibu tawala Mkoa wa Tanga Monica Kinala alishukuru KOICA kwa kuendeleza juhudi za serikali nchini kusogeza mbele elimu na kuwataka wasichoke kuwezesha wananchi elimu ya juu pamoja na ufadhili wa masomo.

Akitoa shukrani kwa niaba wanafunzi, mwenyekiti wa bodi ya wazazi na walezi Salimu Kisauji aliahidi msaada huo kutumika kwa amanufaa ya wengi huku akiiomba KOICA waendelea kuwezesha walimu zaidi wa masomo wa sayansi ambao idadi yao ni haba shuleni hapo.

Shirika la maendeleo ya Korea kusini lina walimu wa kujitolewa 88 wanaofundisha nchini wakiwamo Eun Jung anaefundisha sekondari ya Toledo, Sang Hoon Kim sekondari ya Galanosi, Seung Yoon Choi wa Nguvumali, Jinwon OH wa Msambeni na Song Hyun Mi wa Masechu za jijini Tanga.

No comments:

Post a Comment