HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 11 August 2014

“INAPENDEZA”WANAJUMUIYA YA MOYO MT WA YESU YA PONGWE WATEMBELEA KITUO CHA NYUMBA YA FURAHA CHA JIJINI TANGA NA KUTOA MISAADA MBALIMBALI.



Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Michael Lucas Chikoma akikabidhi misaada katika kituo hicho mbele ya Wanajumuiya wenzake.
Picha ya Pamoja ya Wanajumuiya na Watoto wa kituo hicho kuonesha Upendo na Mshikamano.
Wanajumuiya Mama Toni( kushoto) na Mama Biata(kulia) walionesha mfano mzuri wa Mama mpenda watoto kwa kuwapakata watoto wadogo wa kituo hicho.

Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Michael Lucas Chikoma akiwa amembeba Mtoto aliyeokotwa chooni Pongwe mwezi mmoja uliopita akiwa ametupwa na Mama yake baada ya kuzaliwa, Mtoto huyu analelewa katika kituo hiki akiwa na Afya njema.
Mwanahabari wetu Rebeca Duwe akifanya mahojiano na Sister
Consolata Aloyce
Wanajumuiya Asack na Geofrey wakishusha misaada kutoka kwenye gari.
Na Rebeca Duwe. TANGA
JAMII imeombwa kuwasaidia watu wenye mahitaji na kuwa na bidii ya kuwatembelea watoto yatima wanaoishi kweneye vituo mbalimbali hapa nchini ili wapate Baraka kutoka kwa Mungu.

Haya ameyasema Sister Consolata Aloyce wa kituo cha nyumba ya furaha kilichopo maeneo ya Bombo (Casa Famigria Rosseta) jijini hapa wakati akiongea kwa niaba ya mkurugezi wa kituo hicho Sofia Malera mbele ya Wanajumuiya ya Moyo Mtakatifu wa Yesu kutoka Kigango cha Mtakatifu Gerad Parokia ya Mtakatifu Petro Saruji Pongwe walipowatembelea watoto wa kituo hicho.

Katika hatua nyngine Sister amewataka wale wasichana ambao wanawatupa watoto kwa namna moja ama nyingine waache tabia hiyo, kwani ni  laana katika matumbo yao na hata mbele  za Mungu na wanajitengenezea machinjio kwa kizazi kijacho ndani ya familia yao.
Naye Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Michael Lucas Chikoma amewaasa jamii kuwakaribu na watoto yatima kuliko kujijali wao wenyewe, ili wapate kuwasaidia kwa kuwapa chochote ambacho kinaweza kikawatia moyo katika maisha yao kwani wana uhitaji kama watoto wengine.

Hata hivyo Chikoma  amesma kuwa wale ambao watapata nafasi ya kuwatembelea watoto hao wawe mabalozi kwa wengine kwa ajili ya kuwahamasisha kuja  kuwasaidia watoto yatima walioko kwenye vituo mbalimbali.

No comments:

Post a Comment