HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 29 May 2014

USAFI WA JIJI LA TANGA BADO TATIZO



Bango la Jiji la Tanga  lenye Ujumbe wa Usafi

Uchafu ukiwa umezagaa kwenye soko maarufu la Mgandini jijini humo

WAFANYA biashara wa mazoa ya nafaka na samaki waliopo barabara ya 15 Kata ya Ngamiani Kusini mijni hapa, wameiomba Halmashauri ya jiji la Tanga kusimamia usafi wa mifereji iliyopo kandokando ya barabara hiyo ambayo  imekuwa chanzo kikuu cha kuwepo kwa magonjwa ya milipuko pamoja mazalia ya mbu  hususani kipindi cha mvua.

Wakizungumza na Redio huruma kwa nyakati  tofauti  Akida Ramadhani na Kimaro Gilioni wamesema wao wamekerwa na hali ya uchafu uliopo ndani ya mifereji  hiyo ambayo inasababisha maji machafu kutuama jambo amablo linahatirisha  afya wakazi wa eneo hilo.
Wafanya biashara hao wameiomba Halmashuri kuchua hatua  ya kusafisha mifereji hiyo ili maji yapite kwa uraisi badala ya wafanya biashara kuhangaika wenyewe kuwatafuta vibarua na kuwalipa wenyewe kwa muda mrefu.

Akilizungumzia suala hilo Mwenyekiti wa  Mtaa wa Jamhuri Kata ya Ngamiani Kusini, Shaban Choyo amesema kuwa  ni wajibu wa kila mfanya buiashara kusimamia usafi katika eneo hilo hali ambayo itasaidia  kuondokana na magonjwa ya mlipo kama Dengue na mengineyo.
Amesema yeye kwa kushirikiana na viongozi wengine wa kata watahamasisha jamii zaidi  juu ya usafi huo wa mifereji  kama wanavyo fanya katika maeneo mengine ikiwemo barabarani.

No comments:

Post a Comment