HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 22 May 2014

TAKUKURU TANGA YACHIMBA MKWARA KWA WATOA NA WAPOKEA RUSHWA



Wito umetolewa kwa jamii kuwa ishirikiane na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa ( TAKUKURU)ili kuweza kubaini na kukomesha matukio ya utoaji na upokeaji rushwa mkoani Tanga .

Hayo  yamesemwa na mkuu wa dawati la elimu kwa uma Salome Swai wakati akizungumza na radio huruma ofisini kwake mkoani hapa ambapo amesema kuwa ilikutokomeza vitendo vya rushwa ni wajibu wa kila mtu kutoa taarifa endapo kutakuwa na ushaidi wa kutoa na kupokea rushwa.

Aidha amezitaja kesi walizo nazo kwa mkoa wa Tanga katika mwaka  2013 na 2014 kuwa  jumla ya kesi 56 ikiwa 19 ni mpya na zote zipo mahakamani hii inadhihirisha kuwa vitendo vya rushwa bado vinaendelea.

Hata hivyo takukuru imejipanga katika kubaini na kukuhakikisha wanadhibiti vitendo vyote vya utoaji na upokeaji wa rushwa kwa yeyote atakaye bainika na tuhuma bila kujali umri wala cheo.

No comments:

Post a Comment