HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 23 May 2014

"KUMEKUCHA" MISS TANGA SASA NDIO HABARI YA MJINI "MSHINDI KUCHOMOKA NA GARI YA SH MIL 10


Bi Regina Gwae ( wapili kushoto), Akiongea na wana habari kwa niaba ya kamati ya maandalizi ya Nice and lovely jijini Dar es Salaam kuhusu shindano la miss Tanga linalotarajiwa kufanyika tarehe 21 juni 2014 katika ukumbi wa Mkonge hotel (watatu kulia),Meneja Mauzo Nice and lovely Bw.Brian Kelly.


Bi Regina Gwae (kushoto),akiwaonyesha waandishi wa habari gari lenye thamani ya shilingi milioni 10 kutoka kwa kampuni ya Nice and lovely  litakaloshindaniwa katika shindano hilo (kulia), meneja mauzo wa kampuni hiyo Bw.Brian Kelly.
Wito umetolewa kwa wakazi wa Mkoa wa Tanga na vitongoji vyake kujitokeza kwa wingi kushuhudia shindano kubwa na la aina yake la kuwania taji la urimbwende linalotarajiwa kufanyika tarehe 21 juni 2014 katika ukumbi wa Mkonge hotel.

Akiongea na wana habari kwa niaba ya kamati ya maandalizi ya Nice and lovely Bi Rejina Gwae amesema kuwa wanajivunia kupata nafasi ya kuwa waandaji wa shindano hilo na kutoa wito kwa warembo wote wenye nia ya kushiriki kujitokeza kwa wingi.

Kuhusu zawadi kwa mshindi Bi Rejina amesema kuwa mshindi ataondoka na gari lenye thamani ya shilingi miliono 10 toka kwa kampuni ya Nice and lovely akasema kuwa pia kuna zawadi nyingine za pesa taslimu toka kwa washindi wengine ambazo wanatarajia kuzitangaza baadae.

Kwa upande wake meneja mauzo wa Loreal  wamiliki wa bidhaa za Nice and lovely Briyan Kelly alianza kwa kuishukuru kampuni ya Mac D promotion kwa kuwapa nafasi ya kuwa wadhamini wa nafasi hiyo na kuahidi kuitendea haki nafasi hiyo.

Akamalizia kwa kutoa wito kwa wote wenye nia ya kushiriki katika shindano hilo kujitokeza kwa wingi na kusema kuwa fomu za kushiriki zinapatikana Mkonge hotel, D,boutique tanga mjini,Breez fm,Tanga beach resort, Five brothers, Mwambao fm, Sophia records, Danny fashion barabara ya 13, ofisi za the guardian tanga barabara ya 15 na  Yolanda salon mtaa wa Eckenford na Nyumbani hotel.

No comments:

Post a Comment