HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 30 May 2014

SOKO LA SAMAKI LA DEEP SEA JIJINI TANGA NI SHIDAH..!







Hivi ndivyo Samaki wanavyosafishwa na kuandaliwa kabla ya kuuzwa kwa wateja katika Soko hilo maafufu jiji hapa(picha na Maktaba)


BAADHI ya wachuuzi na wanunuzi wa samaki katika mwambao wa bahari ya hindi eneo la Chumbageni maarufu kama deep see mjini hupa wameilalamikia halmashauri ya jiji la Tanga kwa madai ya kutowawekea mazingira masafi ya kufanyia biashara katika maeneo hayo.

Wakizungumza na mtandao huu kwa nyakati tofauti wanunuzi wa hao wamesema mazingira yaliyopo yamekuwa tishio kubwa kwa afya zao kwa kuhofia kutokea magonjwa ya milipuko kama kipindupindu hasa nyakati za mvua inakuwa vigumu kufika maeneo hayo.

Wamesema kwa sababu ya barabara mbovu ya kuingilia baharini ambayo hujaa tope, wakati mwengeni huteleza na hivyo kushindwa kununua vitoweo.

Akizungumza kwa niaba ya wachuuzi wa samaki wa Deep See, Mohamed Ally amesema mazingira yaliyopo sirafiki kwa afya za watumiaji eneo hilo, hata hivyo ameshangazwa na kitendo cha wao kukatishwa leseni za kufanyia biashara ilihali hakuna huduma za msingi wanazopata kwenye eneo hilo.

No comments:

Post a Comment