HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 22 May 2014

SERIKALI YAWATOA HOFU WANATANGA KUHUSU DENGUE




WIZARA ya afya na ustawi wa jamii, kupitia serikali Mkoani Tanga imekanusha madai ya yanayo enezwa wa wananchi juu ya kuwepo wagonjwa wanaougua homa ya  dengue mkoani hapa.

Akizungumzia uvumi wa kuenea kwa ugonjwa huo Mganga Mkuu Mkoa wa Tanga Asha Mahita, amewaambia waandishi wa habari kuwa may 12 walipokea mgonjwa aliyeonesha dalili za ugonjwa huo hatahivyo baada ya kufanyika vipimo ikaonekana hana ugonjwa huo.

Mahita amesema kuwa hata baada ya kufanyika mawasiliano katika wilaya zote za mkoa wa Tanga tarifa za kitabibu zimethibitisha hakuna mgonjwa aliyedhaniwa kuugua Dengue

Hata hivyo Mganga mkuu amewataka wananchi kutosita kuchunguza afya zao katika vituo vya afya pale inapoonekana dalili za ugonjwa huo na kutilia mkazo umuhimu wa kuendelea kufanyIKa usafi wa mazingira ili kuzuia uwezekano wa mbu wa Aedes anaeambukiza ugonjwa huo kuzaliana.

No comments:

Post a Comment