HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 14 March 2014

WANANCHI WA BUMBULI MKOANI TANGA WAIOMBA SERIKALI KUTATUA MGOGORO WA KIWANDA CHA CHAI MPONDE


MBUNGE WA JIMBO LA BUMBULI  MH.JANUARI  MAKAMBA

SERIKALI imetakiwa kufikia uamuzi wa haraka juu ya kumtafuta mwekezaji mwingine wa kiwanda cha Chai, cha Mponde,  kilichopo Halmashauri ya Bumbuli,  Wilayani  Lushoto, ili kuinusuru chai ya wakulima inayoendelea kuharibikia shambani kwa miezi minane sasa, tangu kifungwe.

Kiwanda hicho cha Mponde ambacho ni Umoja wa Wakulima wa Chai (UTEGA), wanamiliki asilimia hamsini, huku mwekezaji asilimia iliyobaki, kilifungwa baada ya wakulima kugoma kupeleka  majani  mabichi  kwa madai kuwa mwekezaji huyo anawalangua.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wilayani Bumbuli, wakulima hao walisema tangu kiwanda hicho kimefungwa jana chai yao inaharibikia mashambani na kuwapa ugumu wa maisha.

Hamis Jabiri mkulima wa Chai katika halimashauri hiyo, aliiomba serikali kuwafungulia kiwanda chao ili kunusuru maisha yao, maana wamekuwa wakiishi maisha magumu na kuongeza makali ya maisha na kuyumbisha uchumi wao.

Naye Robart Tembe, alisema baada ya kufikia uamuzi wa kukifunga kiwanda hicho, serikali iliunda tume ili kupendekeza kuundwa kwa uongozi wa muda katika kiwanda hicho.

Akizungumzia hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bumbuli, Beatreace Msomisi, alisema tangu kiwanda hicho kilivyoacha kufanya kazi halmashauri hiyo imeathirika kiuchumi, kwasababu ya kiwanda hicho kuwa tegemezi la wakulima.

No comments:

Post a Comment