HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 14 March 2014

MKUU WA MKOA WA TANGA AWAITA WANATANGA NA WALIOSOMA SHULE YA TANGA TECH KUCHANGIA UKARABATI WA SHULE HIYO KONGWE


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Luteni Mstaafu Chiku Gallawa

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa ameitaka jamii na wadau wote wa shule ya Secondari Tanga  Ufundi (Tanga Tech)kufika kwenye mkutano utakao fanyika tarehe 15-3-2014 katika ukumbi wa shule hiyo kuanzia majira ya saa nne kamili asubuhi.

Galawa  ameyasema  hayo wakati  akizungumza  na  kituo hiki ofisini kwake na kusema kuwa lengo la mkutano huo ni kuwakutanisha wanafunzi wote waliowahi  kusoma katika shule hiyo,walimu  waliowahi kufundisha katika shule hiyo pamoja na wadau wote washule hiyo ili kuweza kujadili jinsi yakufanya maboresho ya shule hiyo kongwe na kuiwezesha kuwa na miundombinu ya kisasa ya kujifunzia na kufundishia.

Pia Galawa amesema kuwa jumla ya gharama yote ya miundombinu ni bilionii mbili , milioni 460 laki 6 sitini Elfu na mia6  ambapo awamu yakwanza ya ukarabati inagharimu sh bilioni 1,milioni 400 laki 8 hamsini na sita Elfu na mia sita na awamu ya pili inagharimu kiasi cha sh bilioni 1, 59 milioni laki 7 na Elfu hamsin.

Sambamba na hayo amesema kamati ndogo ya maandalizi imesha pokea msaada wa mifuko 500 ya saruji kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Tanga  cement na shilingi milioni 5 kwa ajili ya ununuzi wa nondo kutoka kwa Mkurugenzi wa Steel rolling industry Tanga nakusema kuwa msaada huo umewezesha kazi ya ujenzi ya uzio wa shule hiyo ianze na mpaka sasa msingi wa ukuta umesha anza kuchimbwa.

Hata hinyo Galawa amemalizia kwa kuwashukuru wadau wote walio changia na wale walio anza kutuma  salamu za udhibitisho wa ushirikiwao katika mkutano huo utakaofanyika Shuleni hapo.

No comments:

Post a Comment