HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 5 March 2014

UONGOZI YANGA WAWAAMBIA WACHEZAJI WAKE LAKI MOJA MOJA ILIKUWA POSHO YA MAFUTA TU, MZIGO WA MAANA MTAPATA BAADAE


Kikosi cha Yanga. Kutoka kushoto waliosimama, Dida,Msuva,Kiiza,Joshua,Yondani,Okwi. Kutoka kushoto walio chuchumaa, Niyonzima,Twite,Cannavaro,Domayo na Ngassa



UONGOZI wa Yanga SC umesema kwamba Sh 100,000 walizopewa kila mchezaji baada ya mechi dhidi ya Al Ahly ya Misri Jumamosi, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam zilikuwa ni posho za mafuta ya gari zao, lakini usiku wa leo watapelekewa posho nzuri baada ya ushindi wa 1-0 siku hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga SC, Mussa Katabaro amesema kuwa anashangazwa na madai ya wachezaji hao kwamba wamepewa posho kiduchu wakati ukweli ni kwamba walipewa fedha kwa ajili ya mafuta ya gari zao.

“Sisi tuna utaratibu wetu tuliojiwekea kwa ajili ya hatua hii na wachezaji wetu watafurahi sana baada ya mechi ya marudiano iwapo wataitoa Al Ahly, siku ile tuliwapa fedha kidogo kama posho ya mafuta ya gari zao, kwa sababu walipewa mapumziko ya siku mbili kabla ua kurudi kambini,”alisema Katabaro.

 

Aidha, Katabaro alisema kwamba uongozi wa Yanga SC jioni ya leo utawapelekea posho nzuri wachezaji wake waliopo kambini hoteli ya Bahari Beach, wakati donge nono linawasubiri baada ya mchezo wa marudiano, wakifanikiwa kuwatoa mabingwa hao wa Afrika.
Pamoja na hayo, habari zaidi kutoka ndani ya Yanga SC, zinasema kwamba wachezaji wote wa klabu hiyo, leo wamelipwa mishahara yao ya Februari- hivyo wataondoka kesho kwenda Misri wakiwa vizuri.

Hivi karibuni baaadhi ya wachezaji wa Yanga SC walinukuliwa na wanahabari wakilalamika morali yao imeshuka kuelekea mchezo wa marudiano na Al Ahly ya Misri Jumapili hii mjini Cairo kuwania kutinga Hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika kwa sababu wamepewa posho kiduchu baada ya mchezo wa kwanza Jumamosi walioshinda bao 1-0.

Lakini juzi, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lilitangaza mapato ‘yaliyogunwa’ kutokana na idadi ya watu kuwa wengi na viingilio vilikuwa vikubwa.  
TFF ilisema mechi hiyo ya Yanga dhidi ya Al Ahly ambao ni mabingwa wa Afrika iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliingiza Sh. 448,414,000.
Kikosi cha Yanga kinatarajiwa kuondoka kesho Dar es Salaam kwenda Cairo tayari kwa mchezo huo wa marudiano Jumapili.

OKWI AKIWAHENYESHA WAARABU




KATIKA HATUA NYINGINE
Beki wa Al- Ahly, Said Ahmed Shedid amesema mechi ya marudiano itakuwa ngumu kwao kutokana na kasi ya washambuliaji wa Yanga pamoja na uwezekano wa mechi hiyo kuchezwa nje ya Cairo na El Gouna.

Yanga na Ahly zitashuka uwanjani Jumapili hii kuumana katika pambano la marudiano la Ligi ya Mabingwa Afrika raundi ya kwanza.
Beki huyo Shedidin alisema pamoja na kubadilishwa uwanja huo bado wanategemea kupata ushindani mkali kutoka kwa washambuliaji wa Yanga wenye kasi kubwa katika kushambulia.

Alisema mechi hiyo itakuwa ngumu kwao kama itachezwa nje ya Cairo na El Gouna, ambako hali yake ya hewa inafanana na ile ya Tanzania.
Kutokana na vurugu zilizojitokeza kwenye fainali ya Kombe la Super Cup kati ya Al-Ahly na CS Sfaxien na kusababisha polisi 22 kuumia, mechi hizo zitachezwa bila mashabiki.

Serikali ya Misri imesema mechi zote za Cairo zitachezwa bila ya mashabiki au kucheza kwenye Uwanja wa Jeshi wa jijini Cairo.
Naye nahodha Mohammad Yousuf, akiuzungumzia mchezo huo wa Jumapili alisema mabingwa hao wa Tanzania wameoneka kuwa wazuri zaidi katika kushambuliajia kwa kasi na kujilinda.

"Nidhamu na kasi yao wanapokuwa na mpira ni jambo inabidi kulifanyia kazi ya ziada kabla ya mechi yetu ya marudiano."
Yousuf alifafanua kuwa mechi hiyo haitakuwa rahisi kwao kutokana na uchezaji wa wapinzani wao. Lakini kurejea kwa nyota wao kama Abdullah Saeed na Sherif Abdul-Fadil ni faida kwao.

Tayari CAF imeshamtangaza mwamuzi wa Badara Diatta kuchezesha mchezo huo akisaidiwa na Jay Haji Abdul Aziz, na Bangor Forbade, na mwamuzi wanne Kebbi Dauda, na msimamizi wa mchezo huo atakuwa Massa Diarra kutoka Mauritania.

Wakati huohuo; Serikali imeitoa hofu Yanga kwa kusema kwamba tayari imechukua hadhari ili kuhakikisha inakuwa salama muda wote itakapokuwa Misri kwa ajili ya pambano dhidi ya Al Ahly.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe akizungumza jijini Dar es Salaam alisema, wizara yake imefanya mawasiliano na Balozi wa Tanzania nchini Misri kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa msafara wa Yanga.

"Nichukue fursa hii kusema kwamba serikali ipo nyuma ya Yanga kwa kuhakikisha inakuwa salama muda wote itakapokuwa Misri kwa ajili ya mechi ya marudiano dhidi ya Al Ahly.
"Tayari wizara yangu imewasiliana na balozi wetu Misri. Watapewa ulinzi mkali na wa hali ya juu kuanzia mazoezini hadi hotelini,"alisema Membe.
Aliongeza:"Lengo ni kuhakikisha timu yetu haifanyiwi vioja au vituko vya aina yoyote itakapokuwa kule, tunataka icheze mechi ikiwa huru."
Tayari uongozi wa Yanga umethibitisha kwamba msafara wa timu hiyo utaondoka nchini kesho kwa ndege ya kuekelea Misri tayari kwa ajili ya mchezo wao.



No comments:

Post a Comment