HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 13 March 2014

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: BARCA, PSG ZAUNGANA NA BAYERN & ATLETICO KUTINGA ROBO FAINALI!!



UEFA CHAMPIONZ LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
MARUDIANO-MATOKEO:
[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
Jumatano Machi 12
FC Barcelona 2 Manchester City 1 [4-1]
Paris Saint-Germain 2 Bayer 04 Leverkusen 1 [6-1]
++++++++++++++++++++++++++++++++++
 
Refa: Stephane Lannoy akimnyooshea kadi nyekundu Zabaleta

BARCELONA 2 MAN CITY 1
Ndani ya Dakika 20 za kwanza Barca, kupitia Neymar, walifunga Bao ambalo lilikataliwa kwa Ofsaidi ambapo marudio yalionyesha Goli ni halali na pia kunyimwa Penati ya wazi baada ya Messi kuchezewa faulo na Lescott.
Kipindi cha Pili, Dakika ya 67, Lionel Messi alifunga Bao kwa Barca baada ya Difensi ya City kujichanganya.
Kwenye Dakika ya 67, City walibaki Mtu 10 pale Zabaleta alipopewa Kadi ya Njano ya Pili alipolalamika kwa Refa kunyimwa kwao Penati wakati Pique alipomkabili Dzeko ndani ya Boksi.
City walisawazisha katika Dakika ya 89 kupitia Nahodha wao Vincent Kompany lakini Barca wakapiga Bao la Pili katika Dakika za Majeruhi baada Andres Iniesta kutumbia kwenye Boksi, kumhadaa Kipa Joe Hart na kumpasia Dani Alves aliewasha kigongo.
Barca wametinga Robo Fainali kwa Jumla ya Bao 4-1.

VIKOSI:
BARCELONA: Valdes, Alves, Pique, Mascherano, Alba, Busquets, Fabregas, Xavi, Iniesta, Messi, Neymar
Akiba: Pinto, Song, Pedro, Alexis, Sergi Roberto, Adriano, Bartra
MAN CITY: Hart, Zabaleta, Kompany, Lescott, Kolarov, Fernandinho, Toure, Milner, Silva, Nasri, Aguero
Akiba: Pantilimon, Clichy, Boyata, Navas, Garcia, Dzeko, Negredo
Refa: Stephane Lannoy (France)

PARIS ST-GERMAIN 2 BAYER LEVERKUSEN 1
Bayer Leverkusen walitangulia kupata Bao katika Dakika ya 6 kupitia Sidney Sam na PSG kusawazisha kwa Bao la Marquinhos Dakika 7 baadae.
Lakini Leverkusen wangeweza kufunga Bao la Pili katika Kipindi cha Kwanza walipopata Penati kufuatia rafu ya Jallet  kwa Derdiyok ambayo Kipa wa PSG, Sirigu, aliokoa vizuri Penati hiyo iliyopigwa na Rolfes.
Dakika ya 54, Lavezzi aliipa PSG Bao la Pili na kufanya Gemu iwe 2-1 na PSG kusonga Robo Fainali kwa Jumla ya Bao 6-1.
VIKOSI:
PSG: Sirigu, Jallet, Marquinhos, Thiago Silva, Digne, Pastore, Cabaye, Rabiot, Cavani, Ibrahimovic, Lavezzi
Akiba: Douchez, Camara, Menez, Thiago Motta, Alex, Maxwell, Lucas Moura.
BAYER LEVERKUSEN: Leno, Donati, Wollscheid, Toprak, Guardado, Rolfes, Reinartz, Can, Sam, Derdiyok, Castro
Akiba: Lomb, Son, Kiessling, Hilbert, Boenisch, Brandt, Wagener.
Refa: Ivan Bebek (Croatia)

UEFA CHAMPIONZ LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
MARUDIANO
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
[Saa za Bongo]
Jumanne Machi 18
22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor Kulübü [1-1]
22:45 Real Madrid CF v Schalke 04 [1-6]
Jumatano Machi 19
22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg [4-2]
22:45 Manchester United v Olympiacos CFP [0-2]
++++++++++++++++++++++++++++++++++
MARUDIANO
MATOKEO:
[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
Jumanne Machi 11
Bayern Munich 1 Arsenal 1 [3-1]
Atletico de Madrid 4 AC Milan 1 [5-2]

No comments:

Post a Comment