HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 12 March 2014

LEO PAPA FRANCIS AMETIMIZA MWAKA MMOJA KATIKA UONGOZI WAKE KWA STAILI YA AINA YAKE




 
Papa Francis


Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki, Papa Francis ametimiza mwaka mmoja tangu alipochaguliwa kushika wadhifa huo.
Katika miezi yake 12 ya uongozi, Papa Francis amefanya mambo kadhaa muhimu ambayo watangulizi wake walishindwa kuyafanya, huku akitoa kipaumbele katika ujenzi wa kanisa hilo katika maeneo yenye ongezeko kubwa la watu na kuwajali masikini.
Papa Francis aliingia madarakani Machi 13, 2013 na kupewa nafasi ya kuliongoza kanisa hilo lenye zaidi ya waumini bilioni 1.2 duniani.

Miongoni mwa mambo yasiyo ya kawaida aliyofanya baada ya kuchaguliwa, ni pamoja na kukataa kutumia gari maalumu kwa ajili yake.
Gari hilo lilikuwa limefunikwa kwa kioo, hivyo kukiuka utaratibu wa awali uliowekwa na Kanisa wa kuwalinda viongozi wao wakuu baada ya Papa John Paul II kupigwa risasi.
Pia Papa Francis aliwahi kusafiri katika basi moja na makadinali. Kama haitoshi, pia alikataa kutumia gari aina ya Mercedes, badala yake alitumia gari aina ya Renault iliyokuwa na miaka 20, huku ikiwa imetembea zaidi ya kilomita laki mbili.

Akielezea aina ya uongozi wake, mwandishi Chris Boeskool anasema uamuzi huo siyo tu ni wa hatari kwa usalama, bali unaonyesha ni namna gani asivyojali kuhusu kifo.
Pia, Papa Francis anaamini kuwa kufanya jambo zuri ni bora kuliko kuamini jambo hilo na kuishia kulisema tu.

“Bwana ametukomboa sisi sote, siyo Wakatoliki peke yao wanaoamini kuwapo kwa Mungu na wasioamini,” aliwahi kusema.
Pamoja na umri wake mkubwa, Papa Francis amekuwa mtumiaji mzuri wa mitandao ya kijamii. Kwa mfano, akaunti yake ya mtandao wa Twitter ina watu zaidi ya milioni tatu wanaomfuatilia duniani kote.

No comments:

Post a Comment