HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 2 March 2014

TAMBWE AIONGOZA MZIMBAZI KUPATA USHINDI WA KWANZA NDANI YA MECHI 5,LIGI KUU BARA

KOCHA WA SIMBA ZDRACO LOGARUSIC





SIMBA SC imezinduka baada ya jioni hii kupata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Katika mchezo huo uliochezwa sambamba na mvua mwanzo hadi mwisho, hadi mapumziko tayari Simba SC walikuwa mbele kwa mabao 2-0.
 
Mrundi Amisi Tambwe aliifungia Simba SC bao la kwanza dakika ya 25 baada ya kuwahi mpira uliotemwa na kipa Abdallah Rashid kufuatia shuti la mpira wa adhabu la Said Ndemla.
WACHEZAJI WA SIMBA ,JONAS MKUDE NA SAID NDEMLA WAKIMPONGEZA KHAMIS TABWE BAADA YA KUIPATIA SIMBA BAO


Tambwe tena alifunga bao lake la 19 msimu huu wa Ligi Kuu dakika ya 33 akiunganisha krosi ya Nahodha Haruna Shamte kutoka kulia.
Kipindi cha pili, Ruvu Shooting inayofundishwa na Mkenya Thom Olaba, ilibadilika kidogo na kufanikiwa kupata bao dakika ya 74, mfungaji Said Dilunga aliyemalizia kona ya Michael Aidan Pius.
Hata hivyo, winga wa Simba SC, Haroun Athumani Chanongo aliifungia timu yake bao la tatu dakika ya 76 baada ya kupata pasi nzuri kutoka kwa Amri Kiemba.
Shambulizi la kushitukiza la Ruvu lilisababisha kizazaa na piga nikupige langoni mwa Simba SC na beki Joseph Owino akaunawa mpira, refa Nathan Lazaro wa Kilimanjaro akamezea, lakini Ramadhani Singano ‘Messi’ akaunawa tena na mwamuzi huyo akatenga tuta, lililokwamishwa nyavuni na Jerome Lambele dakika ya 82. 
Ushindi huo, unaifanya Simba SC ifikishe pointi 35 baada ya kucheza mechi 19 na kuendelea kubaki nafasi ya nne  nyuma ya Mbeya City yenye pointi 36, Yanga pointi 38 na Azam FC pointi 40 kileleni.
KIKOSI CHA WEKUNDU WA MSIMBAZI
Kikosi cha Simba SC leo kilikuwa; Yaw Berko, Haruna Shamte, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Joseph Owino, Donald Mosoti, Jonas Mkude, Haroun Chanongo, Said Ndemla/Ramadhani Chombo ‘Redondo’ dk82, Amisi Tambwe/Abdulhalim Humud ‘Gaucho’ dk78, Amri Kiemba na Ramadhani Singano ‘Messi’.
Ruvu Shooting; Abdallah Rashid, Michael Pius, Mao Bofu, Baraka Jafari, Gedion Sepo, Ali Khan, Hamisi Kisuke/Ayoub Kitala dk46, Juma Nade/Juma Mdindi dk40, Elias Maguri/Jerome Lambele dk61, Said Dilunga na Raphael Kyala.

No comments:

Post a Comment