HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 16 February 2014

WILAYA YA HANDENI YAONA HAYA KUOMBAOMBA CHAKULA, SASA YAHIMIZA WANANCHI WAJIWEKEE AKIBA

MKUU wa wilaya Handeni, Mh Muhingo Rweyemamu


Na Mwandishi Wetu, Handeni
MKUU wa wilaya Handeni, Muhingo Rweyemamu, amesema kwamba ni aibu kubwa kwa wilaya yake kuomba chakula lich licha ya kuzalisha chakula kingi kwa mwaka.
Akizungumza na wanahabari wilayani hapa, Rweyemamu alisema kuwa hali hiyo inampa wakati mgumu, maana wao ni miongoni mwa wilaya zinazoheshimika katika kuzalisha zao la mahindi.
Alisema wafanyabiashara wengi wanaingia Handeni kununua mahindi, hivyo ni wakati wao sasa kuliangalia jambo hilo kwa kina na kuleta tija.
“Kwanza lazima tupige vita kuuza mahindi bila kuweka akiba yetu na familia zetu, maana huo ni mpango mbaya unaotufanya tuombe chakula kila mwaka.
“Nikienda mjini kuomba omba chakula napata wakati kwasababu tuna ardhi ya kutosha na wakulima wetu wengi wanalima, ila mwisho wa siku wanauza hadi akiba za kula wao na watoto wao,” alisema Rweyemamu.
Kwa mujibu wa Rweyemamu, wananchi wote na wakazi wa Handeni wanapaswa walime sana, huku wakijiwekea akiba badala ya kuuza chakula chao, hivyo kuifanya wilaya hiyo ikumbwe na njaa kila wakati.

No comments:

Post a Comment