![]() |
| MKUU WA WILAYA YA HANDENI MHINGO RWEYEMAMU |
SERIKALI
imeombwa kutenga eneo lenye ukubwa wa hekta 2000 kwajili ya kuboresha
mradi wa Ng'ombe wa nyama aina ya Borani na Sewali uliopo katika kijiji
cha Taula Kata ya Kwedizinga Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga.
Akizungumza na wanahabari,Mwenyekiti wa Kampuni ya Masaya Farm Limited Sabas Woiso alisema kuwa matarajio yao ni kufikia hadi Ngombe 1500 wenye tija ambao utawapelekea kuingia katika soko la ndani na nje ya nchi kwa kupitia mradi huo.
Owiso amesema hivi sasa wana eneo dogo ambalo ni hekta 120
ukilinganisha na mifugo iliyopo kuwa mingi na kila ngombe mmoja
anatakiwa kutengewa hekta moja kwa mzunguko wa mwaka tofauti na eneo walilonalo hivi sasa ambapo wana Ngombe 123, Ndama 21 na baadhi yao kuwa wajawazito hivyo itapelekea kuwa na msongamano mkubwa katika eneo hilo.
Owiso amesema kuwa wafugaji wamekuwa wakifuga mifugo yao kwa mazoea hivyo kwa kupitia mradi wao wananchi wa kijiji hicho watajifunza namna ya ufugaji bora na wenye tija kutoka katika maeneo husika sambamba na kupanua soko la Tanzania.
Hata Hivyo Owiso amesema kulingana na mradi huo wananchi wa eneo hilo watafaidika na gesi ya umeme utakaozalishwa kutokana na kinyesi cha Ngombe (Bayogesi), sambamba na kupata ajira, pamoja na kujifunza mbinu za ufugaji bora na wenye tija na kuachana na ufugaji wa mazoea.
"Tukipata eneo la kutosheleza tutaongeza idadi kubwa ya wanyama hawa na tunategemea kujenga uzio ambao utadhibiti afya ya Ngombe huyo ili asipate magonjwa toka kwa ngombe wengine na soko letu litakuwa ndani na nje kulingana na mahitaji husika na kama wadau tutajikita katika kusaidia na kushiriki shuguli za kimaendeleo za kijiji kama vile uchangiaji wa zahanati ya kijiji, Shule, maji, elimu......."alisema Owiso.
Naye Mshauri wa mradi huo Tadei William ameiomba serikali itoe elimu kwa wafugaji wadogo wadogo ili waweze kuondokana na tabia ya ufugaji wamazoea na kujikita katika ufugaji wa kisasa na wenye tija ili aweze kufaidika na ufugaji wake.
William amesema kuwa kupitia elimu hiyo wafugaji watajifunza mbinu za kuachana na ufugaji wa kuhamahama ambao unaharibu mazingira kwa kiasi kikubwa kutokana na mifugo yao kutembea ovyo hali kadhalika itasaidia kuepusha wanyama wasiokuwa na mpangilio maalumu ya mifugo yao.
Mshauri huyo amesema serikali ihamasishe swala la mgao wa upimaji wa maeneo ya wafugaji na wakulima ili kuweza kuwa na mpangilio utakaoweza kuepusha utembeji wa wanyama kiholela na isimamie kwa umakini matumizi bora ya ardhi yatakayoepusha migogoro kati ya wafugaji na wakulima inayorindima siku hadi siku.
Akizungumza na wanahabari,Mwenyekiti wa Kampuni ya Masaya Farm Limited Sabas Woiso alisema kuwa matarajio yao ni kufikia hadi Ngombe 1500 wenye tija ambao utawapelekea kuingia katika soko la ndani na nje ya nchi kwa kupitia mradi huo.
Owiso amesema hivi sasa wana eneo dogo ambalo ni hekta 120
ukilinganisha na mifugo iliyopo kuwa mingi na kila ngombe mmoja
anatakiwa kutengewa hekta moja kwa mzunguko wa mwaka tofauti na eneo walilonalo hivi sasa ambapo wana Ngombe 123, Ndama 21 na baadhi yao kuwa wajawazito hivyo itapelekea kuwa na msongamano mkubwa katika eneo hilo.
Owiso amesema kuwa wafugaji wamekuwa wakifuga mifugo yao kwa mazoea hivyo kwa kupitia mradi wao wananchi wa kijiji hicho watajifunza namna ya ufugaji bora na wenye tija kutoka katika maeneo husika sambamba na kupanua soko la Tanzania.
Hata Hivyo Owiso amesema kulingana na mradi huo wananchi wa eneo hilo watafaidika na gesi ya umeme utakaozalishwa kutokana na kinyesi cha Ngombe (Bayogesi), sambamba na kupata ajira, pamoja na kujifunza mbinu za ufugaji bora na wenye tija na kuachana na ufugaji wa mazoea.
"Tukipata eneo la kutosheleza tutaongeza idadi kubwa ya wanyama hawa na tunategemea kujenga uzio ambao utadhibiti afya ya Ngombe huyo ili asipate magonjwa toka kwa ngombe wengine na soko letu litakuwa ndani na nje kulingana na mahitaji husika na kama wadau tutajikita katika kusaidia na kushiriki shuguli za kimaendeleo za kijiji kama vile uchangiaji wa zahanati ya kijiji, Shule, maji, elimu......."alisema Owiso.
Naye Mshauri wa mradi huo Tadei William ameiomba serikali itoe elimu kwa wafugaji wadogo wadogo ili waweze kuondokana na tabia ya ufugaji wamazoea na kujikita katika ufugaji wa kisasa na wenye tija ili aweze kufaidika na ufugaji wake.
William amesema kuwa kupitia elimu hiyo wafugaji watajifunza mbinu za kuachana na ufugaji wa kuhamahama ambao unaharibu mazingira kwa kiasi kikubwa kutokana na mifugo yao kutembea ovyo hali kadhalika itasaidia kuepusha wanyama wasiokuwa na mpangilio maalumu ya mifugo yao.
Mshauri huyo amesema serikali ihamasishe swala la mgao wa upimaji wa maeneo ya wafugaji na wakulima ili kuweza kuwa na mpangilio utakaoweza kuepusha utembeji wa wanyama kiholela na isimamie kwa umakini matumizi bora ya ardhi yatakayoepusha migogoro kati ya wafugaji na wakulima inayorindima siku hadi siku.

No comments:
Post a Comment