HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 25 February 2014

MKUU WA MKOA ATANGAZA MKAKATI RASMI WA KUBORESHA SHULE YA UFUNDI MKOANI HAPA TANGA



MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA


Mkakati wa kuboresha shule ya ufundi iliopo mkoani hapa umetamkwa rasmi na mwenyekiti wa kamati ya uboreshaji shule hiyo Mkuu wa mkoa wa TANGA Bi Chiku Gallawa katika kikao na waandishi wa habari ofisini kwake.



Gallawa amesema Sekondari ya Tanga ufundi ni shule kongwe nchini yenye historia ndefu tangu enzi za utawala wa kijerumani mwaka 1895 ikiwa katika eneo la awali mkwakwani ambapo kwa sasa ipo shule ya old Tanga.


Kwasasa shule hiyo iko eneo la makorora, ambako imeamishiwa na kufunguliwa rasmi na Rais wa kwanza wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania hayati baba wa Taifa Mwalimu Julias k Nyerere mnamo tar 31/1/1967.


Hata hivyo Gallawa amesema hii ni shule ya kipekee katika historia ya elimu Tanzania kwani ni Sekondari ya kwanza katika nchi hii na imetoa viongozi wengi ikiwa ni pamoja na Rais wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete.



Pia amesema kutokana na umuhimu wa shule hii wameona uko umuhimu wa kukarabati ili kuweza kurudisha shule hii katika historia yake kuienzi na hatimaye iendeleze kutoa wataalamu na viongozi wa ngazi mbalimbali  



Shule hii ina majengo yenye umri 47 na miundo mbinu yake ni ya zamani kwani kwa  muda mrefu  haijafanyiwa ukarabati hivyo kufanya miundo mbinu kuwa katika hali mbaya maeneo yanayo hitaji ukarabati ni madarasa,maabara,

No comments:

Post a Comment