HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 19 February 2014

CLICK HAPA KUPATA HABARI ZA KIMICHEZO



AL AHLY KUIVUTIA KASI YANGA.



WAPINZANI wa timu ya Yanga katika michuano ya Klabu Bingwa ya Afrika, Al Ahly ya Misri watakabiliwa na kibarua kigumu kesho wakati watakapokuwa wenyeji wa timu ya CS Sfaxien ya Tunisia katika mchezo wa kugombea taji la Super Cup utakaofanyika jijini Cairo. Al Ahly itabidi wasahau matokeo mabovu ambayo wamekuwa wakipata katika mechi za ligi ya nyumbani msimu huu kama wanataka kuweka rekodi ya kunyakuwa taji la Super Cup kwa mara ya sita. 

Mechi hiyo ambayo huwakutanisha mabingwa wa Ligi ya Mabingwa msimu uliopita ambao ni Al Ahly na mabingwa wa Kombe la Shirikisho ambao ni Sfaxien unatarajiwa kupigwa katika Uwanja wa Taifa wan chi hiyo uliopo jijini Cairo ambao una uwezo wa kubeba mashabiki 75,000. 

Kocha wa Al Ahly Mohamed Youssef amesema anaamini mechi hiyo ni muhimu kwao kwani itawasaidia wachezaji wake kuongeza kujiaminina kusahau matokeo mabovu yaliyowaandama katika wiki za karibuni. Yanga tayari imeshatuma shushu wake katika mchezo huo ambaye ni kocha msaidizi Charles Boniface Mkwasa kwa ajili ya kuwapeleleza wapinzani wao hao kabla ya mechi yao itakayochezwa Februari 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

FLETCHER AITWA SCOTLAND.



KIUNGO mahiri wa klabu ya Manchester United, Darren Fletcher ameitwa katika kikosi cha timu ya Scotland kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Poland mwezi ujao. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 30 amerejea uwanjani hivi karibuni kufuatia kuugua na anategemewa kuwepo katika mchezo huo utakaochezwa jijini Warsaw Machi 5mwaka huu ikiwa ni mara ya kwanza kuvaa jezi za Scotland toka afanye hivyo mwaka 2012. 

Fletcher ambaye ameichezea Scotland mechi 61, alieleza nia yake ya kutaka kurejea katika majukumu ya kimataifa mara baada ya kupona. nYota huyo aligundulika kusumbuliwa na vidonda vya tumbo mwaka 2011 lakini amefanikiwa kurudi uwanjani baada ya kufanyiwa upasuaji kuondoa eneo lililoathirika.


BAYERN HII SIO KALI KAMA BARCELONA YA PEP GUARDIOLA - 
WENGER.



MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger anaamini kuwa Bayern Munich bado haijafikia kiwango cha Barcelona iliyonyakuwa mataji mawili ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya chini ya kocha Pep Guardiola. Arsenal watakuwa wenyeji wa mabingwa hao wa Ulaya katika mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya leo usiku huku wakiwa na kumbukumbu ya kung’olewa katika hatua kama hiyo na Bayern msimu uliopita sambamba na Barcelona ya Guardiola mwaka 2010 na 2011. 

Ingawa Guardiola amekuwa kocha wa Bayern hivi sasa, Wenger bado anaamini Barcelona ya kipindi kile bado ilikuwa bora kuliko Bayern ambao msimu uliopita walishinda mataji matatu kwa mpigo. Wenger amesema alikuwa akivutiwa zaidi na Barcelona ya kipindi kile kutokana na kasi ya pasi na mchezo wao ni mategemeo yake hawatakutana na hilo watakapocheza na Bayern.


ARSENAL INAWEZA KUWASHANGAZA BAYERN.



NGULI wa soka wa klabu ya Bayern Munich, Stefan Effenberg anaamini kuwa Arsenal inaweza kuwapa wakati mgumu mabingwa hao watetezi kama watatumia aina ya mchezo wa kushambulia katika mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya utakaochezwa baadae leo. Arsenal watakuwa wenyeji wa Bayern inayonolewa na Pep Guardiola katika Uwanja wa Emirates na kama wakiwafunga Wajerumani hao itakuwa timu ya pili kuifunga Bayern toka Julai 2013. 

Kulingana na wacheza mahiri kama Mesut Ozil, Olivier Giroud na Santi Carzola waliopo katika kikosi cha Arsene Wenger, Effenberg anaamini kuwa Arsenal inaweza kuwashangaza Bayern katika mchezo huo. Effenberg amesema pamoja na ubora wa Bayern walionao lakini bado wanaudhaifu katika safu yao ya ulinzi na kama Arsenal wakitumia vyema nafasi zao wanaweza kuibuka kidedea katika mchezo huo ingawa bado anawapa nafasi Wajerumani hao.

No comments:

Post a Comment