HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 12 December 2013

PATA TAARIFA ZA UEFA CHAMPIONS LEAGUE HAPA "WENGER AOMBA MUNGU APATE UBWETE, MOURINHO AITAKA GALA!!




ARSENE WENGER, Bosi wa Arsenal, akisikitishwa kukosa kunyakua Nafasi ya Kwanza ya Kundi lao la UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, sasa anaomba Mungu wabahatike kupata ‘ubwete’ katika Droo ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 itakayofanyika Jumatatu Desemba 16.

Arsenal, ambao Jana walichapwa Bao 2-0 na Napoli na kutupwa Nafasi ya Pili huku Nafasi ya Kwanza ikichukuliwa na Borussia Dortmund walioifunga Marseille 2-0 katika Mechi za Kundi F, wanaweza kukutana na moja kati ya Bayern Munich, Barcelona, Real Madrid, Paris St-Germain au Atletico Madrid katika Raundi ya Mtoano ya Timu 16.

+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++ 

WASHINDI WA MAKUNDI
TIMU ZA PILI ZA MAKUNDI
-Manchester United
-Real Madrid
­-Paris St-Germain
-Bayern Munich
­-Chelsea
-Borussia Dortmund
-Atletico Madrid
-Barcelona

-Bayer Leverkusen
-Galatasaray
-Olympiacos
-Manchester City
-Basel
-Arsenal
-Zenit St. Petersburg
-AC Milan


***DROO: Mshindi wa Kundi anapangiwa Timu za Pili za Makundi ila Timu za Nchi moja au toka Kundi moja haziruhusiwi kukutana.

+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++ 

Wenger ametamka: “Kumaliza Nafasi ya Pili kunafanya Droo yetu kuwa ngumu. Katika Miaka mine, mitano iliyopita tumekuwa na Droo ngumu labda Mwaka huu!”

Msimu uliopita, kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16, Arsenal walipangiwa na Bayern Munich na kufungwa Bao 3-1 Uwanjani Emirates na kushinda 2-0 huko Allianz Arena na Bayern kusonga Bao la Ugenini na hatimae kutwaa Ubingwa.


WAKATI HUO HUO, 
Meneja wa Chelsea Jose Mourinho anataka wapangiwe Galatasaray, Timu anayochezea Staa wake wa zamani, Didier Drogba.

Drogba aliondoka Chelsea Juni 2012 baada ya kukaa huko kwa Miaka minane.

Mourinho amesema: “Galatasaray ni wagumu lakini nataka Didier aje hapa na kuhisi ninachosikia.”

Chelsea, kwa kumaliza Washindi wa Kundi E, wanaweza kupangiwa moja kati ya meet Bayer Leverkusen, Galatasaray, Zenit St Petersburg, Olympiakos au AC Milan.

Hata hivyo, Mourinho amekiri yeyote watakayopangiwa, Mechi itakuwa ngumu kwani kila Timu Ulaya ni ngangari.

UCL-Ratiba:

-Raundi ya Mtoano Timu 16: 18/19/25/26 Feb na Marudiano11/12/18/19 Machi

-Robo Fainali: 1/2 Aprili na Marudiano 8/9 Aprili

-Nusu Fainali: 22/23 Aprili na Marudiano 29/30 Aprili

-Fainali: 24 Mei
MATOKEO:
Jumatano 11 Desemba 2013
Galatasaray 1 Juventus 0 [Mechii hii ilianza Jumanne na kumalizwa Jumatano]
FC Schalke 2 FC Basel 0
Chelsea FC 1 FC Steaua Bucureşti 0
Olympique de Marseille 1 Borussia Dortmund 2
SSC Napoli 2 Arsenal 0
FK Austria Wien 4 Football Club Zenit 1
Club Atlético de Madrid 2 FC Porto 0
AC Milan 0 AFC Ajax 0
FC Barcelona 6 Celtic 1
++++++++++++++++++++++++++++++++++

No comments:

Post a Comment